STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 4, 2011

Jokha Kassim akwama kushebeduka

MWIMBAJI nyota wa muziki wa taarab, Jokha Kassim, amesema bado anaendelea kuhangaikia uzinduzi wa albamu yake binafsi ya 'Wacha Nijishebedue' iliyokwamba kuzinduliwa mwaka jana.
Uzinduzi wa albamu hiyo ulikwama katikati ya mwaka jana kutokana na sababu mbalimbali kubwa kukosa wafadhili na wadhamini wa kumpiga tafu.
Jokha, alisema bado hajakata tamaa kwa vile anaendelea kuwasiliana na wafadhili ili kufanikisha uzinduzi huo ndani ya mwaka huu.
"Najipanga kufanikisha uzinduzi wangu ndani ya mwaka huu, naamini Mungu atanisaidia nipata wadhamini wa kunipiga tafu," alisema.
Mwimbaji huyo alizitaja nyimbo zinazounda albamu yake hiyo 'Yamekushinda', 'Meseji za Nini', 'Kinyang'anyiro Hukiwezi', 'Kelele za Mlango' na Wacha Nijishebedue' uliobeba jina la albamu.
"Niliporekodi na kushuti video ya nyimbo zangu nilipata mfadhili na sasa anatafuta wengine watakaonisaidia kwenye uzinduzi wa albamu yangu, hivyo mashabiki wangu wajue kuwa bado ninahangaikia fedha," alisema.
Alisema, baadhi ya nyimbo zake ukiwemo uliobeba jina la albamu zimekuwa zikisikika kwenye vitu mbalimbali vya redio na televisheni na kumpa matumaini kwamba huenda akapata soko atapozindua.

No comments:

Post a Comment