STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 4, 2012

Mfano yaingiza sokoni Jasho la Mnyonge

FILAMU mpya iliyoandaliwa na kampuni ya uandaaji na usambazaji wa filamu ya Mfano Entertainment na kupewa jina la 'Jasho la Mnyonge' imeingizwa sokoni. Mkurugenzi wa kampuni hiyo na mtunzi wa filamu hiyo, Said Muinga 'Dk. Mfano', alisema filamu hiyo yenye ujumbe mahususi kwa jamii kuhusiana na vitendo viovu tayari ipi sokoni katika mikoa mbalimbali. Alisema kuwa filamu hiyo inaonyesha jinsi gani imani haba za kutaka utajiri wa haraka haraka inavyoweza kupelekea mauaji ya kutisha hasa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino). Muinga alisema kuwa kupitia katika filamu hiyo Watanzania watajionea jinsi wanavyoweza kujiingiza kwenye vitendo vya mauaji kwa ajili ya kujipatia utajiri wa haraka kutokana na kudanganywa na waganga 'feki' wa kienyeji. "Tumeingiza sokoni filamu yetu mpya ya 'Jasho la Mnyonge' , hivyo wapenzi wa filamu nchini ambao walikuwa wakiisubiri kwa hamu kubwa wanaweza kuipata kupitia kwenye maduka mbalimbai yanayojihusisha na uuzaji wa filamu, "alisema Muinga ambaye miezi kadhaa iliyopita aliingiza sokoni filamu nyingine ya 'Yai Viza' ambayo inaendelea kufanya vizuri kwa mauzo. Alisema kuwa zoezi la upigaji picha za filamu hiyo lilifanyikia katika maeneo mbalimbali kulingana na ujumbe husika ikiwemo kwenye misitu mikubwa, maeneo ya vijijini na mjini. Muinga alisema kuwa katika filamu hiyo amewashirikisha wasanii 'mastaa' pamoja na chipukizi lakini ambao wamefanya vizuri katika nafasi zao walizocheza.

No comments:

Post a Comment