STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 8, 2012

Kiiza 'awafunika' Okwi, Ssentongo Uganda

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa timu ya Yanga, Hamis 'Diego' Kiiza ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Uganda kwa mwezi Julai akiwafunika nyota wengine wa nchi hiyo mshambuliaji anayeichezea Simba, Emmanuel Okwi. Kwa mujibu wa mtandao wa habari za michezo wa Kawowo, Kiiza anayeichezea pia timu ya taifa ya Uganda 'The Cranes' alitangazwa kuwa mshindi wa tuzo hiyo ya Julai na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini Uganda, USPA. Mtandao huo ulisema kuwa, Kiiza alifanikiwa kupata jumla ya kura 520, pointi 100 zaidi na aliyeshika nafasi ya pili katika uwaniaji wa tuzo hiyo, kinda la timu ya taifa ya vijana U20, Julius Ogwang aliyevuna pointi 420. Imeelezwa Kiiza amefanikiwa kupata tuzo hiyo kutokana na kuiwezesha Yanga kutwaa ubingwa wa Kombe la Kagame, kwa mara ya pili mfululizo, huku ikimfagilia kwamba licha ya kuibebesha klabu yake ubingwa, pia alinyakua kiatu cha dhahabu cha ufungaji bora kwa mabao sita aliyoyafunga. Hata hivyo ukweli aliyenyakua tuzo hiyo ni Said Bahanunzi pia wa Yanga aliyeifunga idadi kama hiyo ya mabao sita akilingana na Taddy Etekiama wa AS Vita, wakati Kiiza alionekana idadi hiyo ya mabao sita kwa kuongezewa kimakosa bao la beki Stephano Mwasika. Mbali na Kiiza na Ogwang, mwingine aliyekuwa katika Tatu Bora ya waliong'ara mwezi Julai ni mchezaji wa mpira wa wavu, Lawrence Yakan wa mabingwa wa michuano ya kimataifa ya Wavu ya Kampala (KAVC), Sport-S, aliyepata kura 415. Mwisho

No comments:

Post a Comment