STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 8, 2012

Mtanzania kuwania taji jipya la IBF/USBA

MTANZANIA Rajabu Maoja anatarajiwa kuwa bondia wa kwanza wa Tanzania kuwania taji jipya la IBF Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi, lililoanzishwa na Shirikisho la Kimataifa la Ngumi za Kulipwa, IBF/USBA. Kwa mujibu wa Rais wa IBF/USBA kwa nchi za Afrika na Ghuba ya Uajemi, Onesmo Ngowi, Mtanzania huyo atapamba ulingoni Septemba 1, mjini Windhoek, Namibia kupigana na bingwa wa nchi hiyo, Gottlieb Ndokosho. Ngowi alisema IBF/USBA limeanzisha taji hilo kwa nia ya kupanua wigo kwa mabondia wa Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuna ya Uajemi kujitangaza zaidi katika mchezo huo kupitia IBF/USBA. "Katika mpango kabambe wa kupanua wigo wa mabondia wa Bara la Afrika na wale wa Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi, IBF.USBA imezindua taji jipya litakalojulikana kama 'IBF Africa, Middle East and Persian Gulf Title'," alisema Ngowi. Ngowi alisema pambano la kwanza la taji hilo linalojulikana kwa kifupi kama IBF/AMEPG, litafanyikia nchini Namibia likimhusisha Maoja na Ndokosho. Alisema pambano jingine linatarajiwa kufanyika katika jiji la Accra, Ghana kati ya bondia Richard Commey wa Ghana anayejifua kwa sasa nchini Uingereza atakayepigana na bondia kutoka Qatar ambayo iko katika Ghuba ya Uajemi. Ngowi ambaye ni Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBC, alisema juhudi hizo za IBF/USBA zinakuja wakati shirikisho hilo limeanzisha programu ya 'Utalii wa Michezo' na kuziteua Tanzania na Ghana kama nchi za mfano kwa kipindi cha miaka mitatu. Aliongeza fura iliyojitokeza ni fursa nzuri kwa mabondia wa Tanzania kuzichangamkia nafasi hiyo kuweza kuwania mataji makubwa na kujitambulisha kimataifa. Ngowi alibainisha kuwa kwa sasa ni mabondia wachache sana wa Tanzania wenye viwango vya juu ukilingamisha na mabondia wa nchi za Ghana, Namibia, Afrika ya Kusini, Uganda, Nigeria na Misri. Aliahidi kuwapatia mabondia wa kitanzania nafasi za kugombea mataji haya kila panapotokea nafasi hizi ili kuweza kufika walipo wenzao. Mwisho

No comments:

Post a Comment