STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 8, 2012

Safari ya Sikinde Marekani 'yaiva'

BENDI ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Sikinde', imesema itaondoka nchini kwenda Marekani, kushiriki matamasha ya kimataifa mara baada ya sikukuu ya Idd inayotarajiwa kusherehekewa mwishoni mwa mwezi huu. Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo alisema mipango ya safari imekamilika ikiwemo kurejea kwa viongozi na wanamuziki wao waliokuwa nchini humo kuweka mambo sawa. Alisema viongozi hao, Hassani Bitchuka 'Stereo' na Ally Jamwaka waliowawakilisha katika mazungumzo juu ya safari hiyo walisharejea na kusema kuwa kila kitu kimeenda sawa na kilichobaki ni kukamilisha mipango ya safari yao. "Kila kitu kimeenda sawa huko Marekani na viongozi na wanamuziki wetu wamesharejea na kwa sasa tunajipanga kwa ajili ya safari hiyo ambayo itafanyika baada ya kumalizika kwa sikukuu ya Idd," alisema. Aliongeza kuwa wakati wakijiweka tayari kwa ziara hiyo, pia bendi hiyo inaendelea na mipango ya kuzimalizia nyimbo mbili zilizosalia katika albamu ijayo sawia na kujiandaa na mpambano wao na watani zao, Msondo Ngoma. Msondo na Sikinde zinatarajiwa kuchuana katika maonyesho mawili yatakayofanyika katika miji ya Dar na Zanzibar wakati wa sikukuu ya Idd.

No comments:

Post a Comment