STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 15, 2012

CAMEROON NJE TENA MATAIFA YA AFRIKA, YATOLEWA NA CAPE VERDE

Cameroon

CAMEROON imekosa tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani kwa mara ya pili mfululizo, baada ya visiwa vya Cape Verde kwa jumla ya mabao 3-2. Jana Camroon imeshinda mabao 2-1 katika mchezo wa marudiano dhidi ya Cape Verde mjini Yaunde.
Ikumbukwe Cape Verde iliilaza Cameroon 2-0 katika mechi yao kwanza, hivyo wenyeji jana walitakiwa washinde si chini ya 3-0 ili kusonga mbele.
Cape Verde sasa imeweka historia kwa kufuzu mara ya kwanza kwenye fainali hizo za kuwania kombe la Mataifa Afrika, zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Katika mechi nyingine ya kufuzu, Ethiopia ilivaana na Sudan ambapo Ethiopia imeibuka na ushini wa mabao 2-0. Katika mechi ya kwanza Sudan ilishinda 5-3. Ethiopia sasa imufuzu kupitia kwa sheria ya bao la ugenini baada ya timu hizo kufungana jumla ya mabao 5-5.
Mechi kati ya Senegal na Ivory Coast ilivunjika juzi baada ya mashabiki wa soka kuzua ghasia wakati wa mechi hiyo mjini Dakar.
Mashabiki hao wa Senegal, waliwasha moto na kuanza kurusha mawe uwanjani wakati Ivory Coast, ilikuwa ikiongoza kwa mabao 2-0, matokeo ambayo yangeiondoa timu yao. Mashabiki wa Ivory Coast, walilazimika kuingia uwanjani ili kukwepa ghasia hizo.
Wachezaji na mashabiki hao wa Ivory Coast walisindikizwa na Polisi wa kupambana na ghasia ambao walirusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya mashabiki wa Senegal.
Ripoti zinasema watu 10 akiwemo Waziri wa Michezo wa Senegal, Hadhi Malick Gakou, walijeruhiwa kwenye vurugu hizo zilizotokea katika Uwanja wa Leopold Sedar Senghor.
Ghasia hizo zilianza wakati mshambuliaji nyota wa Ivory Coast, Didier Drogba, alipofunga bao lake la pili kwa mkwaju wa penalti, huku zikiwa zimesalia dakika 15 mechi hiyo kumalizika.
Kama mechi hiyo ingelimalizika matokeo yakiwa hivyo, Ivory Coast ingeliibuka na ushindi wa jumla wa mabao 6-2 na kusonga mbele.
Shirikisho la Soka Afrika (CAF) halijatoa taarifa yoyote kuhusiana na tukio hilo, lakini maafisa wa Shirikisho la Soka Senegal, wamesema, timu hiyo ya Senegal huenda ikaadhibiwa vikali na CAF.
MATOKEO KAMILI NA TIMU ZILIZOFUZU:
Ethiopia 2-0 Sudan - Addis Ababa
Matokeo ya Jumla: Sudan 5-5 Ethiopia
Ethiopia wamefuzu kwa faida ya mabao ya ugenini
Cameroon 2-1 Cape Verde  -Yaounde-
Matokeo ya Jumla: Cape Verde 3-2 Cameroon
Cape Verde wamefuzu kwa mara ya kwanza fainali zijazo za Afcon 2013 kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-2.
Angola 2-0 Zimbabwe – Luanda
Matokeo ya Jumla: Angola 3-3 Zimbabwe
Angola wamefuzu kwa faida ya mabao ya ugenini.
MECHI ZA JUMAMOSI (Oktoba 13, 2014)
Malawi 0-1 Ghana - Lilongwe
Matokeo ya Jumla: Ghana 3-0 Malawi
Ghana imefuzu kwa mara nyingine
Botswana 1-4 Mali - Gaborone
Matokeo ya Jumla: Mali 7-1 Botswana
Mali imefuzu
Uganda 1-0 Zambia - Kampala
Matokeo ya Jumla: Uganda 1-1 Zambia
Zambia wameshinda kwa penalti 9-8 na kufuzu
Nigeria 6-1 Liberia - Calabar
Matokeo ya Jumla: Nigeria 8-3 Liberia
Nigeria imefuzu
Tunisia 0-0 Sierra Leone - Monastir
Matokeo ya Jumla: Sierra Leone 2-2 Tunisia
Tunisia wamefuzu kwa faida ya mabao ya ugenini
Senegal 0-2 Ivory Coast - Dakar
Mechi imevunjwa kwa sababu ya vurugu za mashabiki
Matokeo: Morocco 4-0 Msumbiji - Marrakech
Matokeo ya Jumla: Msumbiji 2-4 Morocco
Morocco imefuzu

MABAO YA DROGBA YALIVYOCHAFUA AMANI SENEGAL, DAKAR YANUKA MOSHI

Kimenuka... Drogba akilindwa na Polisi wakati akitolewa uwanjani.
Shabiki wa Senegal akidakwa na polisi baada ya kuingia uwanjani wakati Didier Drogba (kulia) akitaka kupiga penati iliyowapa Ivory Coast uongozi wa mabao 2-0 dhidi ya Senegal katika mechi yao ya kuwania kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2013) kwenye Uwanja wa Leopold Sedar Senghor mjini Dakar, Senegal jana, Octoba 13, 2012. (Picha: AP)
Hatari...!  Mashabiki wa 'chama' la kina Drogba wakihaha kujiokoa jana baada ya vurugu kuibuka katika mechi yao dhidi ya Senegal.

Duh...! Kimenuka hadi kitaa.... mashabiki wa Senegal wakikimbia mitaani huku wakiandamwa na mabomu ya machozi baada ya kuzuka kwa vurugu uwanjani jana.

Yaya Toure (kulia) na wachezaji wenzake wa Ivory Coast wakitolewa uwanjani na 'FFU' wa Senegal baada ya vurugu zilizotokea uwanjani jana.


Sasa uwanjani hapakaliki tena...!

Ni vurugu mtindo mmoja baada ya mashabiki wa Senegal kukasirishwa na kipigo cha Ivory Coast dhidi ya timu yao jana.

Wachezaji Ivory Coast wakitolewa uwanjani.

Wachezaji wakitolewa uwanjani wakisindikizwa na polisi baada ya mawe, chupa na vitu mbalimbali  kurushwa uwanjani na mashabiki wenye hasira wa Senegal waliokasirishwa kuona timu yao ikichapwa na kina Drogba.

Mashabiki wa Ivory Coast wakihaha kujiweka pamoja ili kujiokoa jana.



Kimenuka mwanaa... hapakaliki tena uwanjani!


DAKAR, Senegal 
Mechi muhimu ya kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kati ya Senegal na Ivory Coast imefutwa baada ya mashabiki kuvamia uwanja mjini Dakar juzi.

Mashabiki wa wenyeji walianza kwa kuwasha moto majukwaani na kurusha mawe na vitu vingine uwanjani wakati Senegal wakiwa nyuma kwa mabao 2-0, matokeo ambayo yangewatoa katika michuano hiyo.

Mashabiki wa Ivory Coast walikimbilia uwanjani kuepuka mashambulizi.

Mashabiki na wachezaji wa Ivory Coast baadaye walitolewa nje na polisi, ambao walifyatua mabomu ya machozi kuelekea kwenye majukwaa yaliyofurika mashabiki.

Taarifa zimesema kuwa takriban wati 10 -- akiwamo Waziri wa Michezo wa Senegal,Hadji Malick Gakou -- walijeruhiwa katika vurugu hizo kwenye Uwanja wa  Leopold Sedar Senghor.

Vurugu hizo zilitokea baada ya mshambuliaji wa Ivory Coast, Didier Drogba kufunga goli lake la pili kwa njia ya penati, huku zikiwa zimebaki dakika 15 kabla mechi kumalizika. Kabla ya goli hilo la penati lililokuwa la 58 kwake kuifungia Ivory Coast, Drogba alifunga goli la kwanza katika mechi hiyo kwa njia ya 'fri-kiki'. 

Matokeo hayo yangeiwezesha Ivory Coast kuongoza kwa jumla ya mabao 6-2 baada ya kushinda pia kwa mabao 4-2 katika mechi yao ya kwanza.

"Vyakula, vinywaji na chochote kile kilichoweza kurushwa kilirushwa uwanjani, kutoka katika kona tofauti," Chris Fuglestad, mwanafunzi wa Marekani anayesoma mjini Dakar, aliiambia BBC.

Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) bado halijatoa taarifa rasmi kuhusiana na tukiuo hilo. Lakini afisa mmoja wa Senegal alikaririwa akisema kwamba sasa timu yao itafungiwa na Caf.

Wachezaji ndugu wa Manchester City, Yaya na Kolo Toure walikuwamo katika kikosi cha Ivory Coast, na klabu hiyo ya Ligi Kuu ya England ilisema katika taarifa yake kuwa: "Yaya na Kolo Toure wote wako salama baada ya vurugu za mashabiki kuvunja mechi wakati Senegal walipoikaribisha Ivory Coast mjini Dakar."

SOURCE: straikamkali.blogspot.com

No comments:

Post a Comment