STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 28, 2012

Kivumbi cha Ligi ya England kuendelea leo, Aston Villa yaizamisha Reading

WAKATI vinara wa Ligi Kuu ya England, Manchester United ikitarajiwa kushuka dimbani leo kuvaana na West Ham ili kujihakikishia ufalme wa kileleni, Aston Villa yenyewe jana iliizamisha Reading kwa bao 1-0 huku kocha Harry Redknapp akianza kibarua chake QPR kwa kuambulia suluhu dhidi ya Sunderland.
Manchester itaavana na wagoinga nyundo hao kwenye dimba lao la nyumbani la Old Trafford, ikiwa ni siku chache tangu ilipoiizamisha QPR mabao 3-1.
Mashetani hao wekundu wapo kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 30, moja dhidi ya mabingwa watetezi, Manchester City ambao nao leo watashuka dimbani ugenini kuvaana na Wigan, huku LIverpool itakaribishwa na Tottenham na Arsenal kupambana na Eveton.
 Mechi nyingine zinazochezwa leo ni pambano la Southampton itakayovaana na Norwich City, Stoke City dhidi ya Newcastle United, Swansea City itakayopambana na West Bromwich na Clesea itakayoikaribisha Fulham.
Katika mechi zilizochezwa jana kwenye mfululizo wa ligi hiyo maarufu, Aston Villa iliizamisha Reading kwa kuilaza bao 1-0 lililotupiwa kambani na mshambuliaji wake, Christian Banteke katika dakika ya 80 kwa pasi ya Westwood.
Nayo QPR ikiwa chini ya kocha wake mpya, Harry Redknapp ililazimisha suluhu ugenini dhidi ya wenyeji wao Sunderland na kuifanya timu hiyo inayoburuza mkia katika msimamo wa ligi hiyo kufikisha pointi tano.
ratiba kamili ya mechi zinazochezwa leo katiika ligi hiyo ya England ni kama ifuatavyo:

 Chelsea v Fulham 19:45

  • Everton v Arsenal 19:45
  • Southampton v Norwich 19:45
  • Stoke v Newcastle 19:45
  • Swansea v West Brom 19:45
  • Tottenham v Liverpool 19:45
  • Man Utd v West Ham 20:00
  • Wigan v Man City
  • Wachezaji  Nathan Baker wa Aston Villa (kulia) na Jason Robert wakichuana katika pambano lao la jana.



No comments:

Post a Comment