STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 28, 2012

TENGA ASEMA TFF, SERIKALI KUKUTANA KUMALIZA UTATA WA TRA

Tenga


SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF) pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, wanatarajiwa kukutana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa ajili ya kuzungumzia mustakabali mzima wa suala la makato katika michezo mbalimbali.
Hatua hiyo inafuatia TRA kuzifunga akaunti za udhamini wa ligi hiyo kama shinikizo kwa TFF  kulipa makato ya kodi kwenye mishahara ya timu ya taifa ‘Taifa Stars’ tangu kipindi cha kocha Mbrazil Marcio Maximo kwa madai kwamba imekuwa haikatwi kodi za mishahara ya makocha na hivyo kufikia sh milioni 157,407.968.00.
Rais wa TFF, Leodger Tenga amesema leo kwamba kitendo walichokifanya TRA ni jambo la heri kwani kinaonyesha majukumu ya Serikali katika soka.
Alisema ukaribu uliopo sasa baina ya Serikali chini ya Rais Kikwete na soka ni mkubwa kutokana na ukweli kwamba  inachangia kwa kiasi kikubwa kulipa mishahara ya makocha wa timu za Taifa.
Alisema suala hilo linahitaji mazungumzo baina ya pande hizo ili kuweza kulipatia ufumbuzi na hakuna haja ya kuilaumu TRA kwa sababu inafuata taratibu zilinazostahili kwa mujibu wa kanuni.
 “Hawana njia nyingine ya kufanya hivyo ufumbuzi ni sisi ni kukutana na Wizara na TRA ili kulizungumza hili na katika siku mbili hizi tunarajiwa kukutana,”alisema
Tenga aliongeza kuwa TFF haina uwezo wa kulipa fedha hizo na kwamba hela zilizochuliwa si za Shirikisho hilo bali ni za ligi kuu Bara ambazo zimetolewa na wadhamini wake, kampuni ya simu za mkononi,Vodacom kwa maelekezo maalum.
 “Ni jambo nyeti na lazima lifanyiwe kazi, hatuwezi kumlamu mtu na nimatumaini tutakapoketi pamoja tutapata ufumbuzi,”alisema.
Aidha, Tenga alisema wanatarajia kuzungumzia suala la makato ya michezo mbalimbali ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na vilabu kwa muda mrefu.
 “Changamoto za namna hiyo tumekuwa tukizifanyia kazi kwa muda mrefu na ndiyo maana tangu mwaka 2005 asilimia ya makato ya TFF imekuwa ikipunguzwa, nadhani ni kuendelea kuwa na subira.

No comments:

Post a Comment