STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 19, 2012

Kamote kurudiana na Mmalawi Des 29

Kamote akiwa na mataji anayoyashikilia kwa sasa

BONDIA mtanzania ambaye ni bingwa wa Dunia anayetambuliwa na World Boxing Forum, Allan Kamote anatarajiwa kwenda nchini Malawi ili kuzichapa na mwenyeji wake, Osgood Kayuni katika pambano litakalofanyika wiki ijayo.
Kamote aliyetwaa taji hilo la WBF Septemba 28 mwaka huu kwa kumpiga kwa TKO, Mmalawi Wellington Balakasi, atazichapa na Kayuni katika pambano la uzani wa Light raundi 10 litakalofanyika mjini Blantyre siku ya Desemba 29.
Hilo litakuwa pambano la marudiano baina ya mabondia hao kwani Februari mwaka huu walizichapa nchini huo na Kamote kupigwa kwa pointi, kitu "Natarajia kuondoka nchini siku ya Alhamisi kwenda Malawi kupigana na bondia aitwae Osgood Kayuni, ambayo nilipigana naye Februari mwaka huu na kunishinda kwa pointi, sidhani kama nitarudia tena makosa," alisema.
Kamote anayetokea mkoa wa Tanga, alisema anaendelea vema kujiandaa na pambano hilo na ana imani kubwa kurudia kile alichokifanya kwa Balakasi aliyempiga kwa TKO ya raundi ya nne na kutwaa ubingwa huo wa WBF.

Mwisho

No comments:

Post a Comment