STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 19, 2012

Nusu fainali Kawambwa Cup kuanza kesho


NUSU fainali za michuano ya Kombe la Kawambwa inayoshirikisha timu za soka za Jimbo la Bagamoyo, inatarajiwa kuanza kutimua vumbi keshokuwa ambao timu nne zilizotiunga hatua hiyo zitachuana kuwania kucheza fainali.
Kwa mujibu wa msemaji wa michuano hiyo inayodhaminia na Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo ambaye pia ni Waziri wa Elimu na Ufundi Stadi, Dk Shukuru Kawambwa, Masau Bwire, timu zilizofuzu hatua hiyo ni pamoja na Beach Boys, Mataya Fc, Chaulu na Matimbwa.
Masau alisema timu hizo zilizofua hatua ya roboi fainali iliyochezwa katika vituo viwili, zitaanza kupepetana katika  nusu fainali zitakazoanza kesho Alhamis kwa pambamo kati ya Chaulu Fc dhidi ya Mataya Fc.
"Nusu fainali ya pili itachezwa siku inayofuata yaani Ijumaa Desemba 21 kwa kuzikutanisha Beach Boys dhidi ya Matimbwa Fc, mechi zote zitachezwa katika uwanja wa Mwanakalenge na fainali itakuwa Jumapili," alisema Bwire.
Bwire alisema katika fainali hiyo, mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Dk. Kawambwa ambaye atakabidhi kombe na zawadi nyingine kwea bingwa na washindi wengine wa michuano hiyo.
Msemaji huyo alisema michuano hiyo iliyoanza Septemba 25 mwaka huu ikishirikisha jumla ya timu 84 kutoka kata saba zilizopo jimbo la Bagamyoto za Dunda, Magomeni, Kiromo, Zinga, Kerege, Yombo na Vigwaza iliandaliwa na Waziri huyo kwa lengo la kuibua na kuendeleza vipaji vya soka ndani ya jimbo hilo na mkoa mzima wa Pwani.

Mwisho

No comments:

Post a Comment