STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 20, 2013

Redd's Miss Bagamoyo kusaka vipaji J'5

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiiTkXB_wLHpzsqQ905DvOw1PsYZJNU3Ck8iLgJFN1ZnUWcUQqOMWOIhW8at7WeZnDFjQvkb5NMknVzRipc0RkeX1K4Qgw4_o_DKoNowHCFhbIz1EMhJtfFwNdhQty1eZMVrGlXQv3L2xo/s1600/ROSE+MIS+REDDS.jpg
Redd's Miss Bagamoyo wa mwaka jana.

WAREMBO 10 waliojitokeza kushiriki kinyang'anyiro cha kumsaka Redd's Miss Bagamoyo 2013 wanatarajiwa kuonyeshana kazi kwenye onyesho maalum la kusaka vipaji baina yao litakalofanyika siku ya Jumatano jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa shindano hilo, Awetu Salim ambaye ni Mkurugenzi wa Asilia Decorations, aliiambia MICHARAZO kuwa, shindano hlo la kusaka vipaji litafanyika kwenye ukumbi wa Mikocheni Center (MRC) ambapo burudani mbalimbali zitakuwepo kusindikiza mchuano huyo.
Awetu alisema onyesho hilo linafanyika siku mbili kabla ya warembo hao wanaoendelea na mazoezi yao mjini Bagamoyo hawajakutana kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka mrembo mkali baina yao siku ya Ijumaa kwenye shindano la Redd's Miss bagamopyo litalakalofanyika kwenye ukumbi wa TaSUBA.
"Katika kuwaweka sawa warembo wetu, Jumatano watachuana kusaka mwenye kipaji onyesho litakalofanyika Mbezi, kabla ya Ijumaa kuonyeshana katika katika shindano la kumsaka kisura wa Bagamoyo kwa 2013," alisema Awetu.
Awetu alisema warembo wote 10 watakaochuana kwenye shindano hilo na lile la vipaji wapo fiti na kila mmoja anajitamba kwamba atawafunika wenzake.
Mratibu huyo aliwataja baadhi ya warembo hao watakaochuana ni Juliet Jeremiah, Rose Anthony, Lilian Joseph, Elizabeth Plet, Sulehya Abdi na Fatuma Hamis.

No comments:

Post a Comment