STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 10, 2013

TFF lamchimba mkwara Shafii Dauda kisa barua ya FIFA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgIcvtnmCBqRdmOdMhm1xSloe3lPbWzAf6TIuVarRn2iaYfjrLKFDRXaTZ6FP45x6Txkaxu0GTMf-wMLHf1HSRVsPASI__RtseGcbTrbiQW3z11FugVysqBPtfeQt7wvRCaNWIy1qsSQ6I/s1600/shafi+dauda.JPG
Shafii Dauda akiwa kwenye majukumu yake ya kuwapa wadau wa michezo taarifa kupitia tovuti yake ya www.shafiidauda.com


Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtaka Shaffih Dauda ambaye ni mmiliki wa tovuti ya www.shaffihdauda.com kutoa maelezo kuhusiana na barua ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) aliyoiweka kwenye mtandao wake huo.

FIFA ambayo ilisimamisha mchakato wa uchaguzi wa TFF baada ya baadhi ya wagombea kuulalamikia, baadaye ilitoa maelekezo kuhusu mchakato huo kwa barua ambayo iliituma kwa Rais wa TFF, Leodegar Lenga.

Rais wa TFF katika mkutano wake na waandishi wa habari ambao Dauda alihudhuria alibainisha kuwa barua hiyo ya FIFA hawezi kupewa kila mtu, na kuruhusu waandishi kuisoma kwa Ofisa Habari wa TFF bila kuondoka nayo.

Wakati Rais Tenga anazungumza na waandishi wa habari (Mei 2 mwaka huu), nakala ya barua hiyo ya FIFA ilikuwa kwa viongozi wakuu wa TFF pekee, na viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Hivyo TFF imemtaka Dauda kutoa maelezo ya mahali alipoipata barua hiyo ndani ya siku saba.

No comments:

Post a Comment