STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 10, 2013

Kampira aionya Yanga kwa 'madogo' wa Simba

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgCwx6t_dBA2gr_eCQrTlNALtGAg97uXPt-4TMECmVo7k-QvGveoqvCHiMUxPf8_wW-xczLaqmoUf6Corg3SPn9CIIVhdY9DKMTQQ-KgAgTcrDLJog0Y3hySeSa7bSHScyXJ0uCK3wGThs/s1600/5.jpg
Ramadhani Kampira

 
Baadhi ya 'Yosso' wa Simba wanaomtisha Kampira pambano la Simba na Yanga Mei 18
WINGA wa zamani wa Yanga na TAMCO-Kibaha aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Wilaya ya Kinondoni (KIFA), Ramadhani Yusuph Mzimba 'Kampira', ameionya klabu ya Yanga kuwa inapaswa kuwa makini katika pambano lao na watani zao Simba ili wasiadhiriwe na 'Yosso' wa Msimbazi.
Kampira, ambaye ni mwanachama wa klabu ya Yanga alisema pamoja na kwamba Mabingwa hao wapya wa Ligi Kuu wanaonekana kuwa fiti na kukamilika kila idara, bado wanapaswa kuwa makini na chipukizi wa Simba ili wasiweze kuwatia machungu ya msimu uliopita walipochezea kipigo cha aibu cha mabao 5-0.
Alisema Yanga inapaswa kuingia kwenye pambano la Mei 18 wakiweka dharau kando na kucheza kwa tahadhari kubwa kutokana na ukweli kasi ya vijana wa Simba ambao wameisaidia 'Mnyama' kushinda mechi tatu mfululizo inatisha na kila anayefuatilia soka anaona Yanga itakuwa na wakati mgumu kwa vijana hao.
ke ya Jangwani kuwa makini na vijana wa Simba watakapoumana nao katika pambano la kufungia msimu "Licha ya kwamba Yanga imeshanyakua ubingwa na wanaonekana kuwa bora kuliko Simba msimu huu, bado nilikuwa natoa wito kwa kikosi cha Yanga kushuka dimbani Mei 18, wakiwa na tahadhari kubwa dhidi ya vijana chjipukizi wa Simba, wanaweza kurejesha machungu ya msimu uliopita," alisema Kampira.
Kampira alisema mbali na kuwachunga wachezaji chipukizi wa Simba hasa Haruna Chanongo, Ramadhan Messi, na  Edward Christopher, pia wawe makini na nyota wengine wa Msimbazi walioonyesha wapo juu msimu huu kama Shomar Kapombe, Amri Kiemba na Chollo anayepana na kushuka.
"Nimewaona vijana wa Simba, kwa hakika ni wazuri wanajituma na kujiamini dimbani, kama Yanga itafanya dharau basi yale ya msimu uliopita ya kupigwa mabao 5-0 yanaweza kujirudia, japo naamini msimu huu Yanga imetulia na wakichagiwa na taji walilotwaa kabla ligi haijaisha," alisema Kampira.
Simba na Yanga zitapambana katika pambano la kufungia msimu kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku Yanga wakiwa tayari mabingwa na Simba wakisubiri miujiza kuambulia nafasi ya pili ambayo inaonekana dhahiri inaenda kwa Azam ambayo hata msimu uliopita iliishika nafasi hiyo hiyo nyuma ya Simba.
yanga inaoongoza msimamo mpaka sasa ikiwa na pointi 57, ikifuatiwa na Azam itakayoshuka dimbani Jumamosi kuumana na Mgambo JKT ikiwa na pointi 47 na Simba ipo nafasi ya tatu na pointi zake 45.

No comments:

Post a Comment