STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 23, 2013

Polisi Dar wayanasa majambazi 8 na silaha 7 lakana Mnyika kukoswa na bomu

IMG_9423
Baadhi ya askari polisi wakionyesha kwa waandishi wa habari silaha zilizokamatwa kutoka kwa watuhumiwa wa matukio ya ujambazi.

IMG_9432
DCP Mlege akitoa taarifa ya mafanikio ya Jeshi hilo kwa waandishi wa habari ambapo akizungumzia suala la Mh. Mnyika amesema askari No. E. 5340 D/CPL Julius aliyekuwa ndani ya gari la polisi PT. 1902 alikuwa anasogeza boksi lenye mabomu ya kutoa machozi ya kurusha kwa mkono, kwa bahati mbaya bomu hilo lililipuka ndani ya gari hilo na halikuleta madhara yeyote kwa askari polisi wala raia waliokuwa eneo la uwanja wa Sahara uliopo Mabibo ambako chama cha CHADEMA kilikuwa kifanye mkutano wa hadhara tarehe 21 Jula 2013 kinyume na utaratibu.

Jeshi la Polisi Kanda maalum Dar es Salaam limefanikiwa kukamata sila 5 ikiwemo SMG moja, Shortgun mbili, Riffle Mark 3 tatu, Pisto moja, Risasi 56, Maganda ya Risasi 17 na Majambazi 8.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Kamishna wa polisi kanda hiyo, DCP A.M. Mlege amesema zoezi hilo lilifanyika Julai 18 mwaka huu katika maeneo ya Magomeni wilaya ya Kinondoni.

Amesema pia Jeshi hilo limeweza kukamata magari ya wizi matano, Injini tatu za magari, Vipande vya magari yaliyokatwa spea na wezi watano wa magari.

Katika hatua nyingine Jeshilo limekanusha habari zilizotolewa katika vyombo vya habari kuwa mbunge wa Jimbo la Ubungo Mh. John Mnyika kukoswa na bomu na kumjeruhi mmoja wa wafuasi wake.

Aidha limeomba siku zingine kabla ya kutoa habari ni vizuri likaulizwa ili kuthibitisha au kukanusha.

DCO Mlege amesema pia Jeshi la polisi Kanda maalum Dar es Salaam limemkamata tapeli hatari anayetumia namba tofauti za mitandao ya simu na majina ya watu maarufu anajulikana kwa jina la Mfaume Omari maarufu kama ‘Mau’.

Chanzo - MOBLOG 

No comments:

Post a Comment