STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 27, 2013

Mrisho Ngassa amaliza ubishi, Ruvu Shooting waapa

Mrisho Ngassa
KIUNGO Mrisho Ngassa ameamua kukata mzizi wa fitina baada ya kulipa jkiasi cha Sh. Mil. 45 kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ikiwa ni sehemu ya malipo ya deni alilotakiwa kulipa ili aweze kuitumikia klabu yake ya Yanga

Mkali huyo amelipa deni hilo kama sehemu ya adhabu aliyokuwa amepewa na TFF kwa kosa la kusaini mkataba wa kuichezea Simba kisha kuitosa na kukimbilia Yanga, adhabu nyingine kusimamishwa kucheza mechi sita ambazo alishazimaliza.

Nyota huyo anayeichezea pia timu ya taifa, Taifa Stars baada ya leo kulipa deni hilo sasa Ngassa anaruhisiwa kuanza kuichezea timu yake.

Ngassa anatarajiwa kuanza kuonekana kesho uwanja wa Taifa katika mchezo dhidi ya Ruvu Shooting, ambao wameapa kesho kuendeleza machungu kwa wanajangwani.

Pambano hilo litachezwa kesho ikiwa ni kati ya mechi nne zitakazochezwa katika mfululizo wa Ligi kuu Tanzania Bara.

No comments:

Post a Comment