STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 7, 2013

Zola D 'kuparii in da house' Mombasa

Mkali Zola D katika pozi
NYOTA wa muziki wa Hip hop nchini, David Mlope 'Zola D' amekamilisha wimbo wake mpya uitwao 'Party in da House' na kwa sasa amekimbilia Mombasa Kenya kwa ajili ya kurekodi video yake.
Akizungumza na MICHARAZO, Zola D staa wa nyimbo za 'Moto wa Tipper', 'Rap Gangester', 'Msela Sana' na Jana Siyo Leo', alisema ameamua kwenda kurekodi video hiyo Mombasa kwa lengo la kuipa mandhari tofauti.
Alisema, ndani ya wimbo huo ameimba na 'dogo' aitwaye Man DVD ambaye pia ndiye mzalishaji wa wimbo huo ambao alidai video yake itaachiwa hadharani ndani ya mwezi mmoja ujao baada ya kukamilika kwake.
"Natarajia kuachia 'ngoma' yangu mpya ya 'Party in da House' ambayo nimpigiwa 'chorus' (kibwagizo) na Man DVD na video yake naenda kuirekodia Mombasa Kenya kwa nia ya kuipa ladha na mandhari tofauti na kazi zangu za nyuma," alisema Zola D.
Msanii huyo mwenye 'mwili jumba' na anayejishughulisha pia na mchezo wa ngumi, alisema kazi hiyo mpya ni kati nyimbo zitakazokuwa katika albamu yake ijyao itakayofahamiaka kama 'Swahili Hip Hop'.

No comments:

Post a Comment