STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 8, 2013

Tanzania yazidi kuporomoka FIFA


VIPIGO vinne mfululizo ilivyopata timu ya taifa 'Taifa Stars' imezidi kuiporomosha Tanzania katika orodha ya viwango vya soka duniani ambapo orodha mpya iliyotolewa inaoonyesha ipo nafasi ya 128 toka 121 kwa mwezi uliopita.
Moja wa timu ilizozikwanyua Tanzania katika mbio za kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia, Ivory Coast yenyewe nayo imeporomoka kwa nafasi tano kutoka namba 13 iliyokuwa katika orodha iliyopita hadi kwenye nafasi ya 18 japo inaendelea kutamba barani Afrika ikishika nafasi ya 1.
 ikifuatiwa na Ghana ambao wamesalia nafasi yao ya 24 duniani.
Nchi za Cape Verde imeendelea kupanda chati safari hii kwa nafasi 13 duniani ikikamata namba 36 toka 49 za mwezi uliopita huku barani Afrika ikishika nafasi ya 6 toka ya nane iliyokamata orodha ya awali, huku Cameroon iliyoonekana kuyumba akwa siku za karibu ikipanda kwa nafasi 20 ikishika nafasi ya 51 toka 71 ya awali na Afrika ikishika nafasi ya 8.
Orodha ya jumla ya dunia kwa nafasi za 12 Bora zimesalia kama zilivyo kwa Hispania kuendelea kuongoza ikifuatiwa na Ujerumani, kisha Colombia, Argentina, Uholanzi,  Italia, Ureno, Croatia, Brazili na Belgium, kisha Ugiriki na kumalizwa na Uruguay, huku Marekani wakirejea tena kwwenye Top 20 ya Dunia safari hii.
Orodha kamili mpya ya FIFA unaweza kuipata katika:FIFA World Ranking

No comments:

Post a Comment