STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 8, 2013

Inatisha! Tindikali zahamia kwa wageni

RAIA wawili wa kigeni kutoka katika nchi ya Uingereza ambao wanafanya kazi ya kujitolea katika upande wa ualimu  wamemwagiwa tindi kali mjini Zanzibar jana jioni katika mitaa ya Shangani Mji Mkongwe  visiwani Zanzibar.
Habari kutoka katika chanzo chetu cha habari  kinasema Jeshi la Polisi Zanzibar limeanza msako na kuwatafuta watu waliofanya kitendo hicho dhidi ya walimu hao wa kike waliofika Zanzibar kwa kujitolea kufundisha walitambulika kwa majina ya Kate Gee (18) na Kirsiwer Trup (18) na walikuwa na wiki mbili tu.
Walimu hao waliokutwa na janga hilo walikuwa wanafanya kazi katika shule  moja ya msingi inayojulikana kama Mtakatifu Monika iliyopo chini ya kanisa la Aglicana. habari tulizozipata hivi punde  Raia hao hivi sasa wamehamishiwa katika Hospitali ya Aghakani jijini Dar es salaam kwa matibabu zaid tutazidi kuwaleta habari zaidi.
Tukio hilo limetokea wakati hakuna taarifa zozote za matukio ya nyuma ya kumwagiwa watu tindikali visiwani humo akiwamo Katibu wa Mufti visiwani humo na yale yanayotokea Tanzania Bara maeno ya Dar na Arusha hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment