STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 1, 2013

Tambwe atamba, 'Yanga kitu gani bwana, nitawatungua tu Okto 20'


Amisi Tambwe (kulia) akishangilia mabao yake na Betram Mombeki
MSHAMBULIAJI nyota wa Simba, Amissi Tambwe ameitumia salamu Yanga akiiambia kwamba ikae chonjo kwa ajili ya pambano la watani wa jadi wa soka nchini litakalofanyika Okotba 20, akiahidi kuwatungua ili kuendeleza rekodi yake ya mabao.
Mrundi huyo aliyesajiliwa Simba akitokea Vital'O ya Burundi alisema kwa vile lengo lake ni kufikisha idadi ya mabao 20 mwishoni mwa msimu kitu yoyote itakayokutana na Simba bila kujali kama ni Yanga au Ashanti United akili yake itakuwa kwenye kufumania nyavu tu.
Akizungumza na MICHARAZO leo mara baada ya mazoezi ya klabu yake uwanja wa Kinesi, Tambwe alisema licha ya kwamba hajaiona Yanga ikicheza katika msimu huu, bado anaichukulia kama timu nyingine zilizokutana na Simba ambapo hujitahidi kufunga mabao kwa lengo la kuisaidia timu yake kadhalika kutimiza lengo la kufunga jumla ya mabao 20.
"Sijabahatika kuwaona Yanga wakicheza tangu nitue nchini, lakini nafahamu ni timu kubwa na wapinzani wakubwa wa Simba, lakini hilo mimi sijali siku tutakayokutana nitakuwa na kazi moja tu ya kuwafunga kama ninavyozifunga timu nyingine," alisema.
Alisema yeye awapo dimbani akili zake ni namna ya kujipanga ili kufunga mabao kitu ambacho kimemsaidia kutwaa tuzo kadhaa za ufungaji bora katika ligi yao ya nyumbani na ile ya Kombe la Kagame, kitu anachotaka kitokee pia katika Ligi Kuu ya Tanzania.
Mshambuliaji huyo ambaye alishindwa kuendelea kufanya mazoezi na wenzake kwa kile alichoeleza kusumbuliwa na tumbo, alikiri ligi ya Tanzania ni ngumu na yenye ushindani mkali akidai karibu timu zote zilizocheza na Simba zilionekana kuwakamia kitu anachotarajia hata katika mechi ijayo dhidi ya Ruvu Shooting itakayoyochezwa Jumamosi.
"Ligi ni ngumu na ina ushindani mkubwa, siowezi kusema kuna timu iliyoonekana tishio zaidi ya nyingine ila zote zinacheza kwa malengo na kukamia zaidi, tunashukuru tunaoongoza katika msimamo mpaka sasa," alisema.
na karibu timu zote zina upinzani mkali huku akidai mpaka sasa katika mechi tano alizocheza hawezi kusema timu ipi ilikuwa kali zaidi Mchezaji huyo ndiye anayeoingoza orodha ya wafungaji kwa sasa katika ligi akiwa na mabao saba kutokana na mechi tano alizocheza kwa vile mechi ya awali ya fungua dimba kati ya Simba na Rhion Rangers alikuwa bado hajaruhisiwa kucheza nchini..

No comments:

Post a Comment