STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 1, 2013

Mwenge wa Uhuru wazuia pambano la FDL Iringa

Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya Lipuli ya Iringa na Majimaji ya Songea ambalo lilikuwa lichezwe kesho (Oktoba 2 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Iringa Mjini, sasa utafanyika uwanja wa Wambi Mafinga.

Mabadiliko hayo yamefanyika kutokana na Serikali kuutumia Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora kwa ajili ya shughuli za mbio za Mwenge.

Mechi nyingine ya FDL kesho itakuwa kati ya Tessema FC ya Dar es Salaam na Ndanda FC ya Mtwara, na itafanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment