STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 7, 2013

Kiiza kumkamata Tambwe lna kutimiza ahadi yake leo Taifa?

Hamis Kiiza wa Yanga

Amissi Tambwe wa Simba

Kipre Tchetche wa Azam
MSHAMBULIAJI wa kiganda, Hamis Kiiza 'Diego' hivi karibuni alinukuliwa kwamba angependa kumaliza mechi za duru la kwanza kwa kufunga jumla ya mabao 10, na kabla ya pambano la leo la timu yake ya Yanga dhidi ya Oljoro JKT, tayari anayo mabao nane.
Mabao hayo ni pungufu ya mabao mawili na aliyonayo mkali wa Msimbazi, Mrundi Amissi Tambwe anayeongoza orodha ya wafungaji bora kwa sasa katika Ligi Kuu akiwa na mabao 10, nusu ya mabao aliyoahidi kuyafunga katika msimu wake wa kwanza akiwa na Wekundu wa Msimbazi.
Kiiza, ili kutimiza ahadi yake ya kufunga mabao 10 anapaswa leo kutumbukiza wavuni mabao mawili ambapo mbali na kumkamata mpinzani wake, pia itamfanya kuuaga mwaka 2013 akiwa na furaha na kusubiri kuona mwaka ujao wa 2014 utakuwa wa aina gani kwake na wote wanaokifukizia kiatu cha dhahabu.
Mganda huyo mbali na kutaka kumkamata Tambwe, pia atalazimika kufunga mabao zaidi ikiwezekana ili kumpita Elias Maguri anayeshika nafasi ya pili akiwa na mabao 9 na pia kuwaacha mbali Kipre Tchetche wa Azam mwenye mabao 7 na Juma Luizio wa Mtibwa aliyefunga mabao nane na kulingana naye.
Iwapo atatoka kapa, basi ile ahadi yake ya kufikisha mabao 10 itaambulia patupu na pia kuwaacha wapinzani wake wakimcheka kwa mbaaali kwani itambidi asubiri hadi mwakani panapo majaliwa kuwakimbiza tena.
Wakati Mganda akiwaza hivyo, Kipre Tchetche leo atakuwa na wasaa nzuri wa kuthibitisha kuwa hakubahatika kuwa Mfungaji Bora kwa msimu uliopita wakati atakapovaana na Mbeya City.
Tchetche mwenye mabao saba kwa sasa akishika nafasi ya nne ya wafuingaji inayoongozwa na Tambwe na kufuatiwa na Maguri kisha Kiiza na Luizio, ana kazi nghumu mbele ya Mbeya City ambayo kama ilivyo kwa Azam haijapoteza mechi yoyote msimu huu.
Mashabiki wa soka wangependa kuona 'vita' ya mapro hao ikinoga kama Tchetche atatupia mabao kambani kadfhalika kwa Kiiza na kukimbizana na Tambwe, japo wazawa Muguri na Luizio hawana chao kwa sasa mpaka mwakani kwa vile shughuli yao waliimaliza jana walipozifungia timu zao mabao.
Mbali na mechi za Azam na Mbeya City na ile ya Yanga na Oljoro, leo pia kuna mechi nyingine kati ya Rhino Rangers ya Tabora dhidi ya Prisons Mbeya mechi inayochezwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi ambayo matokeo yake yataweza kuvuruga tu msimamo wa timu zilizopo chini tofauti na mechi hizo mbili za awali ambazo zinaweza kubadilisha taswira ya msimamo wa Tatu Bora wakati ligi ikienda mapumzikoni.
Azam wanaoongoza msimamo ikiwa na pointi 26 sawa na Mbeya City wakizidiana idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa na watetezi Yanga wapo nafasi ya tatu na pointi zao 25 na mechi yao na Oljoro inaonekana kama nyepesi, japo katika soka hakuna kitu kama hicho.

No comments:

Post a Comment