STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 7, 2013

Arsenal, Chelsea zaua, Barca yaichinja Milan, Atletico Madrid dah!

Samuel Eto'o aliyeifungia Chelsea mabao mawili

Ramsey akishangilia bao lake na Mesut Ozil

KOCHA Arsene Wenger huenda sasa anapumua na kuondokana na presha juu ya uwezo wa kikosi chake baada ya usiku wa kuamkia leo kuwatungua Borussia Dotmund ya Ujreumani ikiwa kwao kwa bao 1-0 na kujiweka pazuri kwenye kundi lake katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Bao pekee lililowekwa na kiungo Aaron Ramsey katika dk ya 62, lilitosha kuzima ngebe wa wanafainali hao wa msimu uliopita na kuipa Arsenal ushindi huo na kuifanya ilingane pointi na Napoli walioinyuka Olympique Maseille mabao 3-2 zote zikiwa na pointi 9 na kutofautiana uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jana  Barcelona ikiwa nyumbani iliisulubu AC Milan kwa mabao 3-1, huku nyota wa Argentina,  Lionel Messi akifunga mawili na jingine likizamishwa na Busquets, huku Gerrard Pique akijifunga na kuizawadia wageni bao la kufutia machozi.
Chelsea ilifuata nyayo za Arsenal kwa kuizabua Schalke 04 ya Ujerumani mabao 3-0 kayika pambano lililoshuhudia Samuel Et'oo na mbadala wakem Demba Ba wakifunga mabao hayo yote na kuwapa ushindi muhimu vijana wa Jose Mourinho.
Eto'o alifunga mabao mawili na alipotoka na kuingizwa Ba naye alitupia moja na kufanya Chelsea kutakata ikiwa nyumbani, huku Atletico Madrid ikiwa nyumbani ikiidadavua Viena kwa mabao 4-0, Ajax ikiizima Celtic kwa bao 1-0  na timu za Basel vs Steau Bucharest na Porto na Zenit zikishindwa kutambia katika michezo yao kwa kutoka sare ya baoa 1-1.

No comments:

Post a Comment