STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 6, 2013

MAAFA! WATU SITA WAUWAWA, 35 WALAZWA MAPIGANO YA WAFUGAJI NA WAKULIMA MVOMERO

http://www.herald.co.zw/wp-content/uploads/2013/08/knife-blood.jpg
WATU sita wamefariki baadhi watatu wakiwa wamechinjwa, huku watu wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa vibaya katika mapigano ya kugombea ardhi kati ya wafugaji na wakulima huko kijiji cha Lukindo wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro.
Taarifa zinasema kuwa, chanzo cha vita hivyo ambavyo vimeleta athari kubwa ikiwemo familia kuparaganyika kwa hofu ya mapigano hayo ni mifugo ya wafungaji kuingia katika shamba moja la mkulima na kula mazao.
Baada ya kitendo hicho kilichotokea jana kinaelezwa kuwa, mifugo ya wafungaji ikikamatwa na wakulima na kisha kutaka walipwe fidia ya Sh Milioni 3 na kushindwa kupatikana muafaka kabla ya Polisi kuja kuingilia kati.
Hata hivyo mbele ya polisi makundi hayo mawili yanadaiwa yalianza kupigana mawe na kufanya Polisi walienda kusuluhisha kutimka na ugomvi huo kuibuka upya mapema leo na kusababisha maafa hayo makubwa.
Inaelezwa watu sita wanne wakiwa ni wakulima wameuwawa wengine wakichinjwa kama kuku na wawili wakiwa ni wafungaji na watu 35 wamejeruhiwa vibaya katika miili yao kwa silaha za jadi na kulazwa hospitali ya Bwagala huko huko Mvomero kwa sasa.
Jeshi la Polisi linaelezwa limefanikiwa kutuliza mapigano hayo, lakini watu waliojeruhiwa wakiwa hoi baadhi wakijeruhiwa vibaya na kulazimisha kufanyiwa upasuaji kunusuru maisha yao, ingawa mashuhuda wanasema huenda idadi ya vifo vilivyotokana na mapigano hayo vikaongezeka.

No comments:

Post a Comment