STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 6, 2013

Elias Maguri, Juma Luizio wazidi kukifukizia kiatu cha dhahabu Mtibwa, Ruvu zikitoka sare Mabatini


Juma Luizio 'Ndanda'
MABAO mawili ya mshambuliaji nyota wa Ruvu Shooting, Elias Maguri yaliyoisaidia timu yake kupata sare ya 2-2 na Mtibwa Suigar yamefanya mbio za kuwania kiatu cha dhahabu kuzidi kuwa ngumu baada ya mchezaji huyo kufikisha bao la tisa na kumjongelea Amissi Tambwe wa Simba anayeongoza orodha hiyo.
Maguri amefunga mabao hayo katika pambano la timu yake kufungia duru la kwanza kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi na kuonyesha dhamira yake ya kunyakua kiatu hicho cha dhahabu ambacho msimu uliopita kilichukuliwa na 'Pro' Kipre Tchetche.
Mabao ya wapinzani wao yaliwekwa kimiani na mshambuliaji anayezidi kuja juu nchini, Juma Luizio'Ndanda' ambaye alifikisha bao lake la nane msimu huu na kumfikia Hamis Kiiza huku akibakisha mawili kumkamata Tambwe.
Bao jingine la Mtibwa liliwekwa kimiani na kiungo mzoefu nchini, Shaaban Kisiga 'Marlon' na kuifanya timu yao ya Mtibwa kupata pointi moja na kufikisha pointi 20 na kushika nafasi ya sita ikiipisha Kagera kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

No comments:

Post a Comment