STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 6, 2013

Msiba! DJ RANKEEM RAMADHANI HATUNAYE DUNIANI


KWA mujibu wa taarifa zilizopatikana jioni ya leo, zinaeleza kuwa mmoja wa Ma Dj Maarufu sana hapa jijini Dar na Tanzania kwa ujumla ,Dj Rankeem Ramadhani amefariki mchana huu.
Inaelezwa kuwa DJ Rankeem aliyewahi kufanya kazi Radio One Stereo na vituo vingine mbalimbali alifariki kwenye hospitali ya Mwananyamala baada ya kufanyiwa upasuaji kutokana na tatizo la kidole utumbo.
Mwili wa mkali huyo katika kupangilia muziki aliyetingisha kwa miaka kadhaa, umehifadhiwa kwenye hospitalini hiyo ikifanywa mipango ya mazishi yake.
Taarifa zaidi juu ya msiba huu zitaletwa kwenu kadri tukavyopata kwa undani zaidi ikiwemo kujua atazikwa lini na wapi, ingawa inaelezwa huenda akazikwa kesho jijini Dar es Salaam.
MICHARAZO inatoa pole kwa familia, ndugu jamaa na wadau wote wa habari na muziki kwa msiba wa gwiji hilo, na kuwataka kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu kwa kukumbuka kuwa Sote tu wa Allah (SW) na Kwake Tutarejea.
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi-AMEN

No comments:

Post a Comment