STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 6, 2013

Manchester City yaweka rekodi Ulaya, Juve, Man Utd wabanwa

Aguero akishangulia moja ya mabao yake ya jana kwa CSKA
Bale akiwatungua Juve walipopata sare ya 2-2
 KLABU ya Manchester City kwa mara ya kwanza katika michuano uya Ligi ya Mabingwa Ulaya imevuka salama hatua ya makundi na kuweka rekodi kwao baada ya kuwadungua 'wabaguzi wa rangi' CSKA ya Urusi kwa mabao 5-2 katika pambano kali ya michuano hiyo ya Ulaya.
Mabao mawili ya Sergio 'kun' Aguero na hat trick ya Alvaro Negredo yalitosha kuwavusha wakali hao wa EPL mbele ya Warusi hao.
Bapa la kwanza la Aguero lilitokana na mkwaju wa penati baada ya David Silva kuchezwa vibaya kisha kuongeza jingine kabla ya Negredo kufunga mabao mengine, huku yale ya wageni yote mawili yakifungwa na Doumbia.
Katika mechi nyingine za kundi hilo, Mabingwa watetezi Bayern Munich ilipata ushindi kiduchu wa bao 1-0 na kuendeleza rekodi ya kushindwa kwa asilimia 100 mbele ya Victoria, Juventus ya Italia ikiwa nyumbani ilijitutumua na kuibana Real Madrid na kutoka nao sare ya 2-2, japo walishindwa kuwazuia Cristiano Ronaldo na Bgareth Bale kuwatungua kwani wote wawili walifunga mabao ya wahispania hao.
Manchester United ikiwa ugenini ililazimishwa suluhu na Real Sociedad, huku Shakhtar Doneksk na Bayer Leverkusen nao wakitoka suluhu na mabinhwa wa Ufaransa PSG na Anderletch zikitoka pia sare ya 1-1.
Benfica ikiwa ugenini ililala kwa bao 1-0 kwa Olympiakos na Galatasaray ilikubali kichapo cha ugenini cha bao 1-0 toka kwa Kobenhavn.
Ligi hiyo itaendeela tena usiku wa leo kwa michezo minane baadhi ikiwakutanisha Arsenal itakayokuwa ugenini dhidi ya Borussia Dotmund, Barcelona dhidi ya Ac Milan na Ajax itaikaribisha Celtic.
Mechi nyingine ni kati ya Chelsea dhidi ya Schalke 04, Napoli watakaoumana na Olympique Marseille, Zenit na Porto na Atletico Madrid itakayoumana na Viena.

No comments:

Post a Comment