STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 19, 2013

Emmanuel Okwi kutua rasmi leo akitokea Uganda

Emmanuiel Okwi
 BAADA ya wanachama na mashabiki wa Yanga kuyeyushwa juu ya ujio wa mshambuliaji wao mpya wa kimataifa kutoka nchini Uganda, Emmanuel Okwi, imethibitika kwamba mchezaji huyo atatua leo saa 1:30 kutoka sasa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Yanga muda mcahche uliopita Okwi atatua kwenye uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa MJKN saa 9:30.
Taarifa inasema kuwa Okwi atatu akitokea kwa Uganda kwa Shirika la Ndege la Rwanda na kuwahimiza
wanachama na mashabiki wa klabu hiyo kujitokeza kwa wingi kumlaki.
"Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Emmanuel Okwi anatarajiwa kutua leo mchana majira ya saa 9:30 katika uwanja wa ndege wa Mwalimu JK Nyererer akitokea nchini Uganda kwa shirika la ndege la Rwanda.
Hii ni taarifa rasmi kwa wapenzi wa soka, wanacham na mashabiki kuwa rasmi mchezaji huyo atawasili leo na kupokelewa na viongozi wa klabu ya Yanga pamoja na mashabiki na wanachama kwa ujumla.
Ujio wa Emmanuel Okwi leo unafuatia kukamilisha masuala yake yaliyokuwa yamembakisha nchini Uganda na moja kwa moja leo ataungana na wenzake kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa jumamosi dhidi ya Simba SC katika Nani Mtani Jembe. " Taarifa ya Yanga inasomeka hivyo.

No comments:

Post a Comment