STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 19, 2013

Spurs majanga, Man Utd wakifuzu Nusu Fainali Capital One

Adebayor akishangilia bao lake la jana

Ashley Young akishangilia bao lake dhdi ya Stoke City
TOTTENHAM licha ya kucheza nyumbani ikiwa na kocha mpya, Tim Sherwood ilijikuta iking'olewa kwenye michuano ya Capital One baada ya kunyukwa mabao 2-1 na West Ham United.
Bao la utangulizi la mshambuliaji toka Togo, Emmanuel Adebayor lilishindwa kuilinda wenyeji kuvuka Nusu Fainali bila ya aliyekuwa kocha wake, AVB aliyefurushwa majuzi baada ya kipigo cha mabao 5-0 toka kwa Liverpool.
Adebayor alifunga bao hilo dakika ya 67, lakini mabao ya dakika za jioni kupitia kwa Jarvis na Maiga yaliyotosha kuivusha West Ham United kwenda kuwakabili Manchester City hatua ya Nusu fainali.
Katika mechi nyingine iliyochezwa pia jana usiku, Manchester United ilimpa nafuu kocha wake, David Moyes baada ya kuinyuka Stoke City ugenini kwa mabao 2-0 na kutinga nusu fainali kuwakabili Sundeland.
Mabao ya Ashley Young dakika ya 61 na Patrice Evra dakika ya 78 yalitosha kuwafanya mashabiki wa Mashetani Wekundu angalau kupumua kwa kuwa na hakika ya kunyakua pengine taji hilo kama wataenda vyema baada ya kuonekana kuchechemea kwenye Ligi Kuu msimu huu bila Sir Alex Ferguson.

No comments:

Post a Comment