STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 16, 2014

Du! Luis Suarez azidi kuvuna tuzo England

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Liverpool Luis Suarez amezidi kuongeza tuzo katika kabati lake la kuhifadhia tuzo zake, baada ya kuteuliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu wa 2013-2014.
Nyota huyo aliyefunga mabao 31 na kutoa pasi 12 za mabao katika mechi 33 za ligi alizocheza, huku timu yake Liverpool ikizidiwa kidogo na Manchester City katika mbio za ubingwa, poia ndiye mfungaji bora wa ligi hiyo. 
Suarez, ambaye pia ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Wachezaji wa PFA na Mchezaji Bora wa Waandishi wa habari za Soka msimu huu, ameshinda tuzo ya nne msimu huu pamoja na ile ya kiatu cha dhahabu. 
Tuzo hiyo Suarez imekuja ikiwa ni saa chache baada ya meneja wa Liverpool Brandan Rodgers naye kutunukiwa tuzo ya kocha bora wa mwaka na Chama cha Makocha wa Ligi nchini humo. 
Rodgers amekuwa na msimu mzuri akiiongoza timu hiyo ya Merseyside kumaliza nafasi ya pili kwenye ligi. 
Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson ndiye alimkabidhi tuzo hiyo kocha huyo mwenye umri wa miaka 41, ambayo hutokana na kura zinazopigwa na makocha kutoka timu za madaraja yote manne.
Kabla ya hapo mshambuliaji huyo alikuwa na wakati mgumu kutokana na matukio ya utovu wa nidhamu yaliyomsababisha kufungiwa kucheza mechi kadhaa na kutoza faini kwa kumbagua Patrick Evra na kung'ata beki wa Chelsea.

No comments:

Post a Comment