STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 16, 2014

Simanzi! Amina Ngaluma Japanese afariki ughaibuni

Amina Ngaluma Japanese enzi za uhai wake
TASNIA ya muziki wa dansi imezidi kupata pigo baada ya nyota wa zamani wa bendi za African Revolution 'Tamtam', TOT-Plus na Double M Sound, Amina Ngaluma 'Japanese kufariki dunia.
Mtunzi na muimbaji huyo aliyekuwa akiitumikia bendi ya Jambo Survivors amefariki dunia mchana wa jana akiwa ughaibuni nchini Thailand alipokuwa akifanya shughuli zake za muziki na bendi hiyo.
Taarifa ambazo MICHARAZO ilizipata mapema, zilisema kuwa marehemu alikumbwa na mauti baada ya kuugua ghafla kichwa na kubainika alikuwa na uvimbe uliopasuka na damu kuchanganyika na ubongo.
Baadhi ya wasanii waliowahi kufanya nao kazi, walisema kuwa walipewa taarifa na mume wa marehemu, Rashid Sumuni ambaye ni mcharaza gitaa kuwa mkewe amefariki ughaibuni.
Kifo cha Ngaluma kimetokea wakati wadau wa muziki wa dansi wakiwa hata hawajasahau msiba mzito uliowapata baada ya gwiji Muhidini Mwalimu Gurumo 'Kamanda' kufariki mwezi uliopita.
Mungu ailaze mahali Pema Peponi Roho ya Amina Ngaluma 'Japaness' ambaye alifanyiwa mahojiano na blogu hii miezi michache iliyopita akieleza mipango yake ya kuja kuanzisha bendi na mumewe.
Kwa hakika kila nafsi itaonja mauti, na siku zote kifo hutenganisha wapendanao na kukatisha ndoto za waja, ila kwa kuwa ni kazi ya Mola tunabidi kumshukuru Maanani kwani yeye alimpenda zaidi.

No comments:

Post a Comment