STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 13, 2014

Nyota wa zamani Simba kutimkia Afrika Kusini

David Naftari
BEKI wa zamani wa AFC Arusha na Simba, David Naftar anajiandaa kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya majaribio baada ya mkataba wake na Bandari Kenya ukielekea ukingoni.
Mchezaji kiraka huyo anayemudu nafasi nyingi uwanjani, alisema ataenda kwenye majaribio hayo mara baada ya kumalizika kwa duru la kwanza la Ligi Kuu ya Kenya iliyosaliwa raundi tatu kabla ya kuisha.
Akizungumza na MICHARAZO kutoka Kenya anakocheza soka la kulipwa katika klabu ya Bandari, Naftari alisema mipango hiyo ya kwenda Afrika Kusini inafanywa na wakala wake.
"Japo sijaambiwa nitaenda kujaribiwa katika klabu gani, lakini nitaondoka baada ya ligi kusimama, kwa sasa tumebakisha mechi tatu kabla ya duru hilo kumalizika," alisema.
Kuhusu mktaba wake na Bandari, Naftari alisema unafikia tamati Agosti mwaka huu na tayari viongozi wake wameonyesha nia ya kutaka kumuongezea, lakini mwenyewe hajafanya maamuzi bado.
"Uongozi wa Bandari unaonyesha bado unanihitaji, lakini nataka kwanza niende majaribuni nikirudi nitajua la kufanya kwani mkataba unaisha mwezi wa nane," alisema.
Mchezaji huyo alisema kwa kuwa soka ni maisha yake, daima huwa anapigana kuzidi kusonga mbele zaidi na alipo ndiyo maana hataki kurejea Tanzania kucheza baada ya kuchoshwa na mizengwe.
Naftari alikuwa miongoni mwa wachezaji walioibeba Bandari baada ya kipa Ivo Mapunda, Mohammed Banka na Thomas Mourice waliorejea nchini na Meshack Abel wanaendelea kuichezea mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment