STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 13, 2014

Shinji Kagawa aitwa kikosi cha Japan WC2014

WACHEZAJI nyota Keisuke Honda na Shinji Kagawa ni miongoni mwa wachezaji 23 walioteuliwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Japan kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Dunia mwezi ujao. Kocha Alberto Zaccheroni ambaye amekuwa kocha wa Japan toka mwaka 2010 amechagua wachezaji 12 wanaocheza soka barani Ulaya na 11 wanaocheza katika Ligi Kuu ya nchi hiyo maarufu kama J League. Honda anayecheza klabu ya AC Milan na Kagawa anayecheza Manchester United wanategemewa kwa kiasi kikubwa na nchi yao katika kuhakikisha wanavuka hatua ya makundi katika kundi C ambapo wamepangwa sambamba na Ivory Coast, Ugiriki na Colombia. Japan kwa kipindi kirefu imeshindwa kuwa na washambuliaji wa kutegemewa na Zaccheroni anatarajia kuwategemea Honda na Kagawa katika kutengeneza nafasi na kufunga mabao mengoi ya timu hiyo katika michuano hiyo.

Kikosi Kamili cha Japan:
Makipa: Shuichi Gonda (Tokyo), Eiji Kawashima (Standard Liege), Shusaku Nishikawa (Urawa Reds)

Mabeki: Masahiko Inoha (Jubilo Iwata), Yasuyuki Konno (Gamba Osaka), Masato Morishige (Tokyo), Yuto Nagatomo (Inter), Gotoku Sakai (Stuttgart), Hiroki Sakai (Hannover), Atsuto Uchida (Schalke), Maya Yoshida (Southampton)

Viungo: Toshihiro Aoyama (Sanfrecce Hiroshima), Yasuhito Endo (Gamba Osaka), Makoto Hasebe (Nuremberg), Keisuke Honda (Milan), Shinji Kagawa (Manchester United), Yoichiro Kakitani (Cerezo Osaka), Hiroshi Kiyotake (Nuremberg), Manabu Saito (Yokohama F Marinos), Hotaru Yamaguchi (Cerezo Osaka)

Washambuliaji: Shinji Okazaki (Mainz), Yoshito Okubo (Kawasaki Frontale), Yuya Osako (1860 Munich)

No comments:

Post a Comment