STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 13, 2014

Kikosi cha England hiki hapa, wapo Jack Wilshere, Cole atemwa

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson ametua kikosi cha wachezaji 23 atakaowatumia kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia akiwajumuisha nyota wawili wa Arsenal Jack Wilshere na Alex Oxlade-Chamberlain pamoja na kuwa majeruhi. 
Wilshere alirejea uwanjani katika mchezo wa mwisho dhidi ya Norwich jana baada ya kukaa nje toka Machi baada ya kuumia kifundi cha mguu wa kulia wakati akiwa katika majukumu ya kimataifa. 
Oxlade Chamberlain yeye alikosa nusu ya kwanza ya msimu kwa kuuguza goti na bado kuna hati hati Arsenal wakamkosa katika mchezo fainali ya Kombe la FA kutokana na majeraha kigimbi. 
Pamoja na hayo meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema Hodgson hapaswi kujali sana afya za wachezaji hao kwani bado kuna mwezi mmoja kabla ya Kombe la Dunia hivyo wana muda wa kutosha wa kupona kabisa. 
Kwa upande mwingine chipukizi kama Luke Shaw, Ross Barkley na Raheem Sterling wote wamepata nafasi ya kuwepo katika kikosi cha Hodgson.

Kikosi kamili cha Uingereza ni:
Makipa: Joe Hart (Manchester City), Fraser Forster (Celtic), Ben Foster (West Brom)

Mabeki: Glen Johnson (Liverpool), Phil Jones (Manchster United), Phil Jagielka (Everton), Gary Cahill (Chelsea), Chris Smalling (Manchester United), Luke Shaw (Southampton), Leighton Baines (Everton)

Viungo: Steven Gerrard (Liverpool), Frank Lampard (Chelsea), Jordan Henderson (Liverpool), Ross Barkley (Everton), Jack Wilshere (Arsenal), Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Raheem Sterling (Liverpool), Adam Lallana (Southampton), James Milner (Manchester City)

Washambuliaji: Daniel Sturridge (Liverpool), Wayne Rooney (Manchester United), Danny Welbeck (Manchester United), Rickie Lambert (Southampton)

Wachezaji za ziada :
John Ruddy (Norwich City), John Stones (Everton), Jon Flanagan (Liverpool), Tom Cleverley (Manchester United), Michael Carrick (Manchester United), Jermain Defoe (Toronto), Andy Carroll (West Ham)

No comments:

Post a Comment