STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 13, 2014

Rodgers wa Liverpool, Tony Pullis watwaa tuzo England

RODGERS AKIKABIDHIWA TUZO YAKE
KOCHA wa Liverpool, washindi wa pili wa Ligi Kuu ya Engalnd, Brendan Rodgers ameshinda tuzo ya kocha bora kuliko wote nchini England.
Tuzo hiyo maarufu kama LMA hutolewa baada ya makocha katika madaraja yote nchini humo kupiga kura kumchagua nani ni bora zaidi.
PULLS AKIPEWA TUZO
Pamoja na Liverpool kushika nafasi ya pili lakini Rodgers amekuwa kocha wa Liverpool kushinda tuzo hiyo.
Wakati kocha huyo wa Liverpool akibeba tuzo hiyo ya juu zaidi, Tony Pulls wa Crystal Palace amekuwa kocha bora wa Ligi Kuu England.
Hii maana yake, Rodgers ni bora kwa England kwa kujumuisha na ligi zote ikiwemo Ligi Kuu England wakati Pulls ni kocha wa ligi hiyo moja tu.

No comments:

Post a Comment