STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 13, 2014

Homa ya Dengue yampitia Pentangone wa Twanga

MUIMBAJI wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta', Ramadhani Mhoza 'Pentagone' ameongeza idadi ya wasanii waliokumbwa na ugonjwa mpya wa homa ya Dengue baada na kulazwa hospitalini kutokana na kuugua ugonjwa huo unaofanana na Malaria.
Pentagone alikumbwa na ugonjwa huo wiki iliyopita na kulazwa hospitalini kwa siku tatu kabla ya kupata nafuu na kuruhusiwa kwenda kujiuguzia nyumbani kwake, ambako kwa sasa anaendelea vyema.
Akizungumza na MICHARAZO akiwa mapumziko nyumbani kwake, Pentagone, alisema hakuwa anajua lolote kuhusu ugonjwa huo mpya hadi alipokimbizwa hospitalini baada ya kuumwa kichwa, kuhisi uchovu na kuumwa kwa viungo vya mwili na alipopimwa na madakatari aligundulika kuambukizwa homa hiyo mpya inayozidi kushika kasi kwa sasa nchini.
Pentagone alisema anashukuru kwa sasa anaendelea vyema japo bado hana nguvu na anaamini wakati wowote atarejea tena jukwaani kuungana na wanamuziki wenzake.
"Namshukuru Mungu naendelea vyema, nilikuwa hoi hospitalini kutokana na hii homa mpya iitwayo Dengue, kwa sasa sina nguvu tu mwilini, lakini naendelea vyema," alisema.
Kuugua kwa Pentagone kumefanya idadi ya wasanii waliokumbwa na homa hiyo kufikia watatu kwa sasa baada ya awali mwanadada Rehema Chalamila 'Ray C' kuthibitishwa kuugua ugonjwa huo na kulazwa hospitali sawa na ilivyomkuta pia, Mukhsen Awadh 'Dk Cheni na muigizaji mkongwe ambaye kwa sasa ni mtangazaji wa Times Fm, Susan Lewis 'Natasha'.
Ugonjwa huo unaelezwa kuambukiwa na mbu aina ya Aedes unafanana kwa kiasi kikubwa na ugonjwa wa Malaria kwa dalili zake na watu wanaohisi kuupata wanahimizwa kuwahi hospitalini kupata matibabu.

No comments:

Post a Comment