STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 13, 2014

Hiki ndicho kikosi cha Black Stars, wamo Essien, Boateng

KIUNGO nyota wa AC Milan, Michael Essien na Kevin-Prince Boateng wamejumuishwa kwenye kikosi cha awali cha wachezaji 26 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia.
Kikosi hicho kitapunguzwa na kubaki wachezaji 23 baada ya mchezo wa kirafiki na Uholanzi Mei 31, ambacho ndiyo watakwenda Brazil.
Essien na Boateng wameitwa baada ya kurejea kwenye soka ya kimataifa mwaka jana, kufuatia awali kuomba kujipumzisha kuichezea timu hiyo.
Nchi ya Ghana imepangwa kundi moja na timu za  Marekani, Ujerumani na Ureno likitajwa kuwa ni moja ya makundi ya kifo katika fainali za mwaka huu zitakazoanza mwezi ujao nchini Brazili.

Kikosi kamili cha Black Stars ni kama kifuatavyo:
Makipa: Stephen Adams (Aduana Stars), Fatau Dauda (Orlando Pirates), Adam Kwarasey (Stromsgodset)
 
Mabeki: Harrison Afful (Esperance), Jerry Akaminko (Eskisehirspor), John Boye (Stade Rennes), Samuel Inkoom (Platanias), Jonathan Mensah (Evian Thonon Gaillard), Daniel Opare (Standard Liege), Jeffrey Schluup (Leicester City), Rashid Sumaila (Mamelodi Sundowns)
 
Viungo: David Accam (Helsingborg), Afriyie Acquah (Parma), Albert Adomah (Middlesbrough), Emmanuel Agyemang Badu (Udinese), Kwadwo Asamoah (Juventus), Christian Atsu (Vitesse Arnhem), Andre Ayew (Olympique Marseille), Michael Essien (AC Milan), Rabiu Mohammed (Kuban Krasnodar), Sulley Muntari (AC Milan), Mubarak Wakaso (Rubin Kazan)
 
Washambuliaji: Jordan Ayew (Sochaux), Kevin Prince Boateng (Schalke 04), Asamoah Gyan (Al Ain), Abdul Majeed Waris (Valenciennes).

No comments:

Post a Comment