STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 5, 2015

Aibu! Watanzania 443 wanaswa na dawa za kulevya ughaibuni

http://api.ning.com/files/NWvFMlVPFcx5SxCYa4RDXr0NMMnq6gRcpSfjyInB*mxa*WWMz0x1MendQbi7EkT588mJKfgz3DjGsbaCvcR6Q0AgTJ03rTXA/Pipi.jpg
Baadhi ya dawa zilizowahi kunaswa nchini
http://api.ning.com/files/NGHxxVgVd17fuWKh*v1l7*4NyFc2GYTkLp2o69tup7nXuo4nQgBPU2OuQ-it1jCnSiXwKCGVj6KQ*c8ylkYzAyOgRGizDiJb/IMG_0532.jpgBIASHARA ya Dawa za Kulevya bado ni kizungumkuti kwa taifa la Tanzania, kwa raia wake wapatao 443 kunaswa katika mataifa mbalimbali duniani.
Hata hivyio ni angalau udhibiti juu ya biashara hiyo nchini imeanza kuonekana kwa kunaswa kwa 'unga' upatao tani 2.3 (kilo 2300).
Imeelezwa kuwa Tanzania imefanikiwa kudhibiti zaidi ya tani 2.3 za dawa za kulevya zilizokamatwa na vikosi vya wanamaji huku za zaidi ya watanzania 443 wamekamatwa katika nchi mbalimbali duniani wakihusishwa na usafirishaji na utumiaji wa dawa za kulevya. 
Akizungumza jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa ripoti ya dawa za kulevya ya Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Kudhibiti Dawa za Kulevya na Makosa ya Jinai (UNODC) Mwakilishi kutoka Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini Tanzania Bw. January Ngisi amesema tatizo la dawa za kulevya katika ukanda wa Afrika Mashariki bado ni kubwa na kueleza kwa kushirikiana na vyombo vya dola wameridhia mikataba ya kupunguza upatikanaji wa dawa za kulevya.
Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Bi. Stela Vuzo amesema ripoti hiyo imeitaka serikali kuwasaidia watoto wasijingize katika matumzi ya dawa za kulevya ambazo zimekuwa na madhara makubwa ikiwemo athari za kiafya na iwekwe mikakati itakayotokomeza uingizwaji na utumiaji wa dawa za kulevya nchini.

No comments:

Post a Comment