STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 8, 2015

AFCON 2017 KAZI KWELI, STARS WAPEWA MISRI, NIGERIA

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/07/TAIFA1.jpg
Taifa Stars
Kombe la AFCON
SAFARI ya Taifa Stars ya Tanzania katika mchakato wa kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) zitakazofanyika nchini Gabon mwaka 2017, inaonekana kuwa ngumu. Hii ni baada ya  Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kuipanga kundi moja la G pamoja na vigogo.
Kwa mujibu wa droo iliyofanyika jana jijini Cairo, Misri, Tanzania imepangwa kundi moja na mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo, Misri, pia wakipewa mabingwa wa mwaka jana, Nigeria na Chad. Huku Morocco, Tunisia zilizokuwa zimefungiwa na CAF nazo zikijumuishwa katika droo hiyo.
Timu 16 zitakazopenya katika hatua hiyo ya makundi ndiyo watakaoenda Gabon kusaka ubingwa ambao kwa sasa unashikiliwa na Ivory Coast waliotwaa mapema mwaka huu kwa kuilaza Ghana.
Tanzania kwa mara ya kwanza na mwisho kufuzu fainali hizo ilikuwa mwaka 1980 wakati michuano hiyo ilipofanyika nchini Nigeria na kwa miaka zaidi ya 30 imekuwa ikisota kusaka nafasi ya kushiriki tena bila mafanikio.
Makundi ya michuano hiyo ambayo awali ilikuwa iandaliwe na Libya kabla ya hali ya machafuko ya kisiasa kuifanya ijitoe ni kama yafuatavyo;
Kundi A: Tunisia, Togo, Liberia, Djibouti
Kundi B: Madagascar, DRC, Angola, CAR
Kundi C: Mali, Equatorial Guinea, Benin, South Sudan
Kundi D: Burkina Faso, Uganda, Botswana, Comoros
Kundi E: Zambia, Congo, Kenya, Guinea Bissau
Kundi F: Cape Verde, Morocco, Libya, Sao Tome
Kundi G: Nigeria, Egypt, Tanzania, Chad
Kundi H: Ghana, Mozambique, Rwanda, Mauritius
Kundi I: Cote d'Ivoire, Sudan, Sierra Leone, Gabon
Kundi J: Algeria, Ethiopia, Lesotho, Seychelles
Kundi K: Senegal, Niger, Nambia, Burundi
Kundi L: Guinea, Malawi, Zimbabwe, Swaziland
Kundi M: Cameroon, South Africa, Gambia, Mauritania

No comments:

Post a Comment