STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 27, 2011

Bingwa wa Kick Boxing Kenya atua Bongo kuzipiga




BINGWA wa Kick Boxing kutoka Kenya, Rukia Kaselete ametua nchini tayari kwa ajili ya pambano lake dhidi ya Mtanzania Jamhuri Said, watakaosindikiza pambano la nani mkali kati ya Amour Zungu wa Zanzibar na Mchumia Tumbo wa Tanzania Bara.
Michezo hiyo iliyoandaliwa na Bingwa wa Dunia wa Kick Boxing anayeshikilia mikanda ya WKL na WKC, Japhet Kaseba inatarajiwa kucheza siku ya Jumamosi kwenye ukumbi wa DDC Keko, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Kaseba, alisema maandalizi ya michezo hiyo kwa wastani inaendelea vema ikiwemo mabondia wote kuwasili jijini akiwemo mkenya huyo atakayepigana na Jamhuri kusindikiza pambano la Zungu na mwenzake.
Kaseba alisema mabondia wote watakaoshiriki michezo hiyo ya Kick Boxing na Ngumi za Kulipwa wanatarajiwa kupimwa afya zao siku ya Ijumaa kwenye gym yake, iliyopo eneo la Mwananyamala jijini Dar es Salaam.
"Kwa kweli kila kitu kinaenda vema ikiwemo mabondia wote kuwasili Dar tayari kwa ajili ya michezo hiyo ya Jumamosi, ambapo Amour Zungu atazipiga na Mchumia Tumbo katika pambano la kusaka mkali kati yao," alisema Kaseba.
Kaseba alisema mbali na pamoja ya pambano la Kaseleta na Jamhuri, siku hiyo pia kutakuwa na michezo mingine ya utangulizi ambapo wanadada Asha Abubakar wa Kisarawe na Fadhila Adam wa Dar wataonyeshana kazi kwenye kick boxing.
"Wengine watakaopigana siku hiyo ni kati ya Dragon Kaizum dhisi ya Faza Boy, Idd na Dragon Boy na Lion Heart ataonyeshana kazi na Begeje," alisema.
Aliongeza pambano la ngumi za kulipwa zitawakutanisha wakongwe wa mchezo huo, Ernest Bujiku dhidi ya Maneno Osward 'Mtambo wa Gongo'.

Mwisho

No comments:

Post a Comment