STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 27, 2011

Talent Band kutambulisha mpya Sinza

BENDI ya muziki wa dansi ya Talent 'Wazee wa Kuchechemea' inatarajiwa kuvamia kitongoji cha Sinza ili kuitambulisha albamu yao mpya ya 'Shoka la Bucha'.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Husseni Jumbe, aliambia MICHARAZO jana kuwa, onyesho hilo litafanyika kesho kwenye ukumbi wa Nouvel Social Centre (zamani Rufita) ambapo watatambulisha nyimbo zote zilizopo kwenye albamu hiyo mpya.
Jumbe, alisema onyesho hilo limeratibiwa na Mkurugenzi wa ukumbi huyo aliyemtaja kwa jina la Mamaa Joyce.
"Baada ya kuikamilisha albamu yetu mpya ya Shoka la Bucha, Talent Band, inatarajiwa kuitambulisha albamu hiyo katika onyesho maalum litakaloofanyika siku ya Alhamis kwenye ukumbi wa Nouvel Social Centre," alisema Jumbe.
Jumbe alizitaja nyimbo zitakazotambulishwa kwenye onyesho hilo kuwa ni Shoka la Bucha, Kiapo Mara Tatu, Kilio cha Swahiba na zile za albamu yao ya kwanza ya Subiri Kidogo.
Naye mratibu wa onyesho hilo, Joyce alisema kila kitu kipo sawa na wanachosubiri ni kupata burudani toka kwa Talent.

Mwisho

No comments:

Post a Comment