STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 31, 2011

Siujasaini kokote-Nsa Job





MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Yanga, Nsa Job, amedai hajasaini kokote hadi sasa licha ya jina lake kuwepo kwenye orodha ya wachezaji wa klabu ya Villa Squad.
Hata hivyo mchezaji huyo, alisema kama uongozi wa Villa utakaa nae mezani na kukubaliana juu ya masilahi atakubali kuichezea kwa vile imeonyesha nia ya kumhitaji.
Akizungumza na MICHARAZO, Job, aliyeachwa na Yanga msimu huu baada ya kuitumikia msimu uliopita akitokea Azam, alisema hakuna mazungumzo yoyote aliyofanya na Villa waka kusaini kuichezea klabu hiyo.
Alisema, mara alipoachwa na Yanga alikuwa kwenye mipango ya kwenda Sweden kucheza soka la kulipwa, hivyo hakuwahi kufanya mazungumzo na klabu yoyote, ila kama ni kweli Villa inamhitaji ataweza kuwasaidia wakielewana juu ya suala la masilahi.
"Sijasaini kokote ndugu yangu, sio Villa wala klabu nyingine niliyofanya nao mazungumzo, ila kama klabu hiyo inanitaka sioni tatizo kuichezea kama tutaelewana juu ya masilahi, si unajua soka ni ajira bwana," alisema Job.
Mshambuliaji huyo aliyewahi kuzichezea Moro United na Simba, alisema hata kama atakubaliana na Villa kuichezea, bado mipango yake ya kwenda kucheza soka la kulipwa ipo pale pale kwani anaendelea kuwasiliana na wakala wake Nyupi Mwakitosa.
Job, alisema wakala huyo ambaye ni mchezaji wa zamani wa soka Tanzania mwenye uraia wa Sweden kwa sasa, amemhakikishia kumhangaikia kupata timu ya kwenda kufanya nanyo majaribio baada ya ile ya awali kushindwa kukubaliana nao baadhi ya mambo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment