STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 31, 2011

Super D aachia DVD nyingine za kufunzia ngumi




KOCHA maarufu wa mchezo wa ngumi nchini, Rajab Mhamila 'Super D' aliyeamua kutumia njia ya DVD kuwafunza watu ngumi, ameachia kazi nyingne tatu mpya.
Kazi hizo tatu zinahusisha mapambano kadhaa ya nyota na mabingwa wa ngumi za kulipwa duniani, ziachiwa sokoni zaidi ya wiki moja sasa.
Akizungumza na MICHARAZO, Super D, alisema tofauti na kanda yake ya awali, DVD za sasa zimeandaliwa kisasa na zikiwa na mchanganyiko wa 'clips' za michezo ya nyota wa dunia katika kuwafunza watu namna ya kupigana ngumi.
Super D, alisema mbali na michezo ya nyota hao wa dunia akiwemo Manny Pacquiao, Floyd Maywather, Roy Jones na wakali wengine DVD hizo pia zina michezo ya tamasha lao la ngumi wanaloendesha kwa kushirikiana na kocha Habib Kinyogoli.
"Katika muendelezo wa kuwafunza watu ngumi kwa njia rahisi, nimetoa dvd pamoja na cd nyingine tatu tofauti zilizokusanya michezo ya mabingwa wa dunia na mafunzo ya ngumi tunayoendesha kupitia tamasha letu na Kinyogoli Foundation," alisema.
Super D, ambaye ni kocha wa klabu ya ngumi ya Ashanti, alisema anaamini kupitia njia hiyo watu wengi wenye kupenda kujifunza mchezo wa ngumi kwa kuangalia mbinu na ufundi katika mchezo huo kupitia michezo ya mabondia waliopo kwenye dvd hizo.
Aliongeza kuwa, mbali na dvd hizo bado vijana wenye vipaji vya ngumi wanaweza kujiunga na klabu zao za Ashanti na Amana kujifunza 'live' chini ya makocha Habib Kinyogoli, Kondo Nassor, yeye Super D na wengine wanaowanoa vijana mbalimbali.

Mwisho

No comments:

Post a Comment