STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 31, 2011

Kalapina ahubiri Uzalendo nchini

MSANII nyota wa muziki wa hip hop nchini, Karama Masoud 'Kalapina' ametaka somo la uzalendo lifunzwe rasmi shuleni kwa nia ya kuwapika viongozi na wananchi watakaokuwa na uchungu wa kweli dhidi ya nchi yao kitu kinachoweza kupunguza ufisadi.
Kalapina, alisema somo hilo la uzalendo mbali na kusaidia kuondoa ufisadi, pia itawafanya hata wasanii kujipenda na kujithamini kwa kutanguliza utanzania kwanza tofauti na sasa kukosa kujiamini na kuendelea kuwatukuza wasanii wa kigeni na kushindwa kuwika kimataifa.
Akizungumza na blog hii mwishoni mwa wiki, Kalapina alisema mambo yanayoendelea nchini kuanzia kwa wananchi wa kawaida hadi viongozi na wanasiasa kuwa wabinafsi, wenye uchu na kutokuwa na uchungu wa nchi yao imetokana na kukosekana kwa somo la uzalendo.
"Nadhani watanzania tangu utotoni wakianza kufunzwa uzalendo na kujithamini wenyewe, vitendo vya ufisadi, uharamia na wasanii kupenda kuwaiga wasanii wa kimataifa badala ya kubuni kazi zao litaondoka na nchi itaenda vema," alisema.
Kalapina, alisema hata vitendo vya wanajamii kuwaibia kazi wasanii unatokana na ukosefu wa uzalendo na kuzidi kuwafanya wasanii kuendelea kuishi maisha ya dhiki kinyume na wenzao wa kimataifa wanaoongoza kwa utajiri kuliko hata viongozi wao wa serikali.
Kiongozi huyo wa kundi la muziki wa hip hop la Kikosi cha Mizinga, alisema hapendi hali ya mambo inayoendelea nchini kwa watanzania kuwa maskini wakati inafahamika nchi ina rasilimali zinazoweza kuwafanya waishi maisha ya kitajiri kuliko taifa lolote barani Afrika

No comments:

Post a Comment