STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 19, 2016

Mavugo kimeeleweka, kuivaa Ndanda Taifa

Mavugo
Na Tariq Badru
UHONDO unakolea. Klabu ya Simba imepata hati ya uhamisho wa kimataifa  (ITC) za mastraika wake wawili wa kigeni, Laudit Mavugo na Frederic Blagnon.
ITC hizo zimetua leo Ijumaa mchana baada ya kukamilisha uhamisho wao na sasa wanaweza kuanza majukumu yao Msimbazi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyopostiwa kwenye mitandao na Katibu Mkuu wa Simba, Patrick Kahemele ni kwamba ITC  zimetua nchini leo mchana kutoka katika mashirikisho ya soka ya Burundi na Ivory Coast.
Blagnon Fredric Goue ametokea klabu ya Africa Sports ambao ni wapinzani wa jadi wa ASEC Mimosas ya nchini Ivory Coast.
Wakati Mavugo yeye anatokea klabu ya Vital'O ya Burundi na kupatikana kwa hati hizo kunamaliza utata wa uhamisho wa Mavugo ambaye kulitokea kwa maneno toka kwa uongozi wa klabu ya Vital’O kuwa bado ana mkataba wa mwaka mmoja jambo ambalo lilikanushwa na Mavugo.
Mavugo amewakuna mashabiki wa Simba baada yab kupiga mpira mwingi kwenye mechi ya Tamasha la Simba Day dhidi ya AFC Leopards ya Kenya na ile mechi ya URA.

No comments:

Post a Comment