STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 19, 2016

Duh! Liverpool yaukacha Uwanja wao wa Anfield mwezi mzima


LIVERPOOL iliyoanza vema Ligi Kuu ya England msimu huu kwa kuikandika Arsenal kwa mabao 4-3 inatarajia kucheza mechi zake tatu zinazofuata ikiwa ugenini kitu ambacho si cha kawaida.
Sababu inayoifanya Liverpool isicheze kwenye Uwanja wao wa Anfield kwa mwezi mzima na kucheza mechi tatu mfululizo za EPL ugenini ni kwa sasa ni kutokana na ombi lao wenyewe la kutaka uwanja wao ukarabatiwe.
Mechi inayofuata kwa Liverpool ni kesho Jumamosi ikivaana na Burnley ugenini, lakini imebainika kuwa wametaka hivyo ili kupisha kukamilika kwa ujenzi wa upanuzi wa Jukwaa Kuu la Uwanja wao wa Anfield.
Jukwaa hilo limepanuliwa na kuongezwa ngazi 3 juu za kukalia mashabiki, kupanua ukumbi wa Wachezaji kuingia na kutoka uwanjani kutoka vyumba vya Kubadili Jezi, mabenchi ya wachezaji wa akiba na Jopo lao la Ufundi kutengenezwa upya. Pia sehemu maalum kwa walemavu itatengenezwa upya sambamba na kuboreshwa kwa miundo mbinu ya watazamaji.
Jukwaa Kuu la Anfield litaongeza viti 8,500 na kuufanya Uwanja huo sasa uingize jumla ya Watazamaji 54,000.
Mechi ya kwanza kabisa kwa Liverpool kukanyaga Anfield Jijini Liverpool msimu huu itakuwa Septemba 10 watakapovaana na Mabingwa Watetezi Leicester City.

No comments:

Post a Comment