STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 19, 2016

KUMEKUCHA VODACOM PREMIER LEAGUE 2016-2017

Mabingwa watetezi Yanga
Simba
Azam
NA RAHIM JUNIOR
MSIMU mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom Premier League, VPL unatarajiwa kuanza rasmi kesho Jumamosi kwa michezo mitano, huku mtetezi Yanga ikila shushu hadi Agosti 31 kwa vile ina majukumu ya kimataifa.
Yanga inatarajiwa kuondoka siku ya Jumapili kwenda Lubumbashi nchini DR Congo kumaliza mchezo wake wa kukamilisha ratiba ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji TP Mazembe itakayochezwa Jumanne ijayo.
Kwa mujibu wa ratiba ya VPL, kesho kuitakuwa na michezo itakayohusisha Simba ambayo itaialika Ndanda ya Mtwara kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, huku Azam itakuwa mwenyeji wa African Lyon Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Mjini SHinyanga kwenye Uwanja wa Karambage, Stand United itakwaruzana na Mbao FC ya Mwanza inayoshiriki ligi hiyo kwa mara ya kwanza, wakati Mtibwa Sugar itaikaribisha Ruvu Shooting ya Pwani kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani mjini Morogoro.
Mechi nyingine itazihusisha Maafande wa Prisons ya Mbeya itakayosafiri hadi mjini Songea, Mkoa wa Ruvuama kuvaana na wenyeji wao Majimaji kenye Uwanja wa Majimaji.
Ligi hiyo itaendelea Jumapili kwa mchezo mmoja tu,  Kagera Sugar itaialika Mbeya City kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga kabla ya Jumatano
Toto Africans haijavaana na Mwadui kwenye uwanja wa CCM Kirumba. Mechi hizo zimehamishiwa hapo kwa vile Uwanja wa Kaitaba, Bukoba bado haujakamilika kukaratabiwa na ule wa CCM Kirumba kuwa na kazi nyingine likiangushwa Tamasha la Fiesta 2016.
Ligi hiyo inaanza huku karibu timu zote zimefanya usajili wa maana na baahi kubadilisha benchi la ufundi la timu zao.
Klabu nne pekee ndizo ambazo zinashiriki ligi hiyo zikiwa na makocha wao wa msimu uliopita na zilizosalia zimebadilisha kwa kuwaleta wapya ama kubadilishana na wapinzani wao kama ilivyo kwa Mtibwa Sugar na Kagera Sugar.
Kocha Mecky Maxime aliyekuwa Mtibwa ametua Kagera Sugar na nafasi yake kuchukuliwa na Salum Mayanga aliyekuwa akiinoa Prisons Mbeya.
Makocha wengine wapya katika ligi hiyo ni Zeben Hernandez kutoka Hispania anayeinoa Azam, Joseph Omog wa Simba, Rogasian Kaijage wa Toto Africans na Etienne Ndeyirageji wa Mbao FC anayetokea Burundi.
JKT Ruvu iliyosukwa upya pia ina kocha mpya Hamis Malale 'Hamsini' aliyekuwa Ndanda wakati Ndanda sasa inanolewa na Joseph Lazaro aliyekuwa Mgambo JKT iliyoshuka daraja, huku Ruvu Shooting ikiwa na kocha mpya Seleman Mtingwe.
Africna Lyon naye inashiriki ligi hiyo baada ya kurejea kutoka Ligi Daraja la Kwanza ikiwa na kocha wa zamani wa Simba, Dragan Popadic akisaidiwa na Ramadhani Aluko, huku Majimaji Songea ikiwa chini ya Kocha Juma Mhina.
Mbali na makocha msimu huu utashuhudia vikosi vinavyoundwa na wachezaji wapya waliosajili kwenye timu hizo shiriki gumzo likiwa ni usajili wa straika kutoka Burundi, Laudit Mavugo na wakali wengine ndani ya kikosi hicho akiwamo, Shiza Kichuya, Federick Blagnon, Method Mwanjali na Mussa Ndusha.
Je, unadhani ni timu ipi itaanza msimu na mguu mzuri? Tusubiri baada ya dakika 90 za mipambano hiyo na ile ya kesho.


Ratiba ilivyo:
Kesho Jumamosi
Simba            v Ndanda
Stand Utd       v Mbao
Mtibwa Sugar v Ruvu Shooting
Azam             v African Lyon
Majimaji         v Prisons

Jumapili

Kagera Sugar v Mbeya City

Jumatano

Toto African    v Mwadui
 


No comments:

Post a Comment