STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 19, 2016

Pogba kuanza mambo yake Man United

KAZI imeanza. Kiungo mpya wa klabu ya Manchester United, Paul Pogba leo Ijumaa anatarajiwa kuanza kuitumikia timu yake hiyo kwa mara ya kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Southampton.
Pogba aliyeondoka klabuni hapo kwa mlango wa nyuma mwaka 2012 kwenda Juventus amerejea tena Man United kwa ada ya Pauni Milioni 89 iliyovunja rekodi ya dunia, alishindwa kuanza katika mchezo uliopita dhidi ya Bournemouth.
Kilichomkwamisha nyota huyo wa Ufaransa kukipiga kwenye mchezo huo ambao Man Un ited ilishinda mabao 3-1 ni kwa sababu ya kutumikia adhabu ya mechi moja aliyotoka nayo Italia katika Ligi ya Serie A.
Akihojiwa kuhusu mchezo wa leo usiku, Pogba alisema anajisikia yuko fiti na amekuwa akifanya mazoezi kwa siku 10, lakini hata hivyo itategemea meneja wake Jose Mourinho atakavyoona inafaa.
Pogba aliendelea kudai kuwa ameshazoea hali hiyo kwani amekuwa akifanya mazoezi hata wakati alipokuwa likizo hivyo anajiona yuko sawa.
Man United itaivaa Saints ikitegemea safu yake kuongozwa na nyota wao mpya, Zlatan Ibrahimovic aliyeanza kwa makeke ndani ya klabu hiyo inayoongoza msimamo kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Hata hivyo mapema leo mchana Kocha Mourinho aliwahakikishia mashabiki wa Man United kuwa kiungo Paul Pogba atawavaa Southampton.
Kocha Mourinho alisema Pogba amefanya mazoezi kwa siku 11 na imekuwa rahisi kumbadili Pogba kwa vile ni kijana aliyekulia OT na anamjua kila mtu.
Alipoulizwa kama yeye anaweza kusaidia kurejesha ile hali ya timu kuiogoga Man United iliyokuwepo enzi za Sir Alex Ferguson, Mourinho alijibu: “Sio mimi. Ni timu, ndio. Na mashabiki pia. Nadhani kila kitu kinaanza hapo, uhusiano kati ya timu na mashabiki.”
Aliongeza: “Ikiwa humo Old Trafford, mashabiki wa upinzani, maelfu kadhaa wanakuwa na kelele kubwa kupita Mashabiki zaidi ya 70,000, basi sisi tupo mashakani. Inamaanisha uhusiano kati ya timu na mashabiki wake. Kukiwepo uhusiano, basi ule ukweli wa kutisha tukiwa nyumbani utarudi. Kila kitu kinaanza na uhusiano huo wa timu na mashabiki wake. Ikiwa mashabiki watahusiana na timu, wanataka nao kucheza na wakicheza, wapinzani hawana nafasi!”
Kwa taarifa yako tu ni kwamba Southampton imekuwa ikizoa pointi tatu kwenye Uwanja wa Old Trafford kwa misimu miwili sasa wakifungamana na Norwich City, Swansea City na West Bromwich Albion.


No comments:

Post a Comment