STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 23, 2012

Msondo Ngoma kupeleka mpya Masasi, ikienda kuzindua ukumbi wa Emirates

BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma, inatarajiwa kuipeleka albamu yake mpya ya 'Suluhu' mjini Masasi, Mtwara watakapoenda kuzindua ukumbi mpya mjini humo. Msemaji wa Msondo, Rajabu Mhamila 'Super D' alisema bendi yao itaenda kuzindua ukumbi huo uitwao Emirates, siku ya Juni 2 ambapo watatumia nafasi hiyo kutambulisha albamu hiyo mpya na nyimbo zao za zamani. Super D, alisema Msondo imepewa fursa hiyo ya kwenda kuzindua na kutumbuiza ukumbini hapo baada ya maombi ya mashabiki wao wa Masasi kuililia bendi hiyo iende kuwapa burudani. Alisema, msafara wao utaongozwa na mkongwe Muhidini Gurumo 'Kamanda' aliyerejea upya kupanda jukwaani baada ya kitambo kirefu kusumbuliwa na maradhi. "Kamanda Gurumo ndiye atakayeongoza jahazi sambamba na Dokta Said Mabela ambapo tutatambulisha albamu yetu kwa mashabiki hao wa Masasi, sawi na kukumbushia vibao vyetu vya zamani," alisema. Albamu hiyo ya Msondo Ngoma ina nyimbo sita ambazo ni 'Suluhu', 'Lipi Jema', 'Dawa ya Deni', 'Baba Kibene' 'Nadhiri ya Mapenzi' na 'Kwa Mjomba Hakuna Urithi'. Mwisho

No comments:

Post a Comment