STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 23, 2012

Samata, Ulimwengu waiongezea nguvu Stars

Washambuliaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaocheza mpira wa kulipwa katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) wamejiunga na kambi ya timu ya Taifa (Taifa Stars) juzi. Wachezaji hao ambao ndiyo pekee kutoka nje walioitwa na Kocha Kim Poulsen kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia Kanda ya Afrika dhidi ya Ivory Coast itakayochezwa Juni 2 mwaka huu jijini Abidjan waliwasili juzi saa 1.30 usiku kwa ndege ya Kenya Airways. Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inaendelea na mazoezi jijini Dar es Salaam kwenye viwanja vya Karume na Taifa itacheza mechi ya kirafiki Mei 26 mwaka huu dhidi ya Malawi. Mechi hiyo itafanyika Uwanja wa Taifa, na Malawi itawasili nchini Mei 24 mwaka huu. Baadaye Malawi itakwenda Zanzibar kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Zanzibar Heroes itakayofanyika Mei 28 mwaka huu kabla ya kuondoka Mei 30 mwaka huu kwenda Uganda ambapo Juni 2 mwaka huu itcheza mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia Kanda ya Afrika. Katika hatua nyingine, kiungo wa timu hiyo, Nurdin Bakar atalikosa pambano la kirafiki dhidi la Malawi kutokana na kuchanika nyama ya paja hali inayomfanya awe nje kwa wiki moja kabla ya kurejea tena dimbani. Bakari, alipata majeraha hayo katika mazoezi ya timu hiyo inayoendelea kujivua kwenye viwanja vya Karume, Ilala Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment