STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 23, 2012

Azam yapewa 'shavu' Kagame Cup

WASHINDI wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Azam FC watashiriki michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, maarufu kama Kombe la Kagame Julai, mwaka huu, Dar es Salaam, imeelezwa. Kuingia kwa Azam kwenye michuano hiyo, iliyofanyika kwa mara ya kwanza mwaka 1974, kunamaanisha Tanzania Bara, wenyeji watawakilishwa na timu tatu, nyingine zikiwa ni mabingwa watetezi wa Kombe hilo, Yanga na mabingwa wa Ligi Kuu, Simba SC. Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah alisema jana mjini Dar es Salaam kwamba maandalizi ya michuano hiyo, yanaendelea vizuri na tayari wadhamini wamekwishapatikana na watatangazwa katika Mkutano maalum hivi karibuni. Azam inayoshikilia pia taji la Kombe la Mapinduzi, itakuwa ni mara yao ya kwanza kushiriki michuano hiyo mikubwa kwa ngazi ya klabu kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Timu nyingine za Tanzania Bara zitakazoshiriki michuano hiyo ni mabingwa watetezi wa taji hilo, Yanga na mabingwa wapya wa Tanzania, Simba.

No comments:

Post a Comment